• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Arusha Regional

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Mkoa
      • Chimbuko/Asili ya eneo
      • Orodha ya wakuu wa Mikoa
    • Dira na dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji Mali
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Wilaya
    • Arusha
      • Historia
      • Viongozi
    • Arumeru
      • Historia
      • Viongozi
    • Monduli
      • Historia
      • Viongozi
    • Karatu
      • Historia
      • Viongozi
    • Longido
      • Historia
      • Viongozi
    • Ngorongoro
      • Historia
      • Viongozi
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Arusha
    • Halmashauri ya Arusha
    • Halmashauri ya Meru
    • Halmashauri ya Monduli
    • Halmashauri ya Karatu
    • Halmashauri ya Longido
    • Halmashauri ya Ngorongoro
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo
    • Viwanda
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Ardhi
    • Utalii
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali
    • Habari
    • Matukio

RC MONGELLA AWAASA WANAFUNZI SHULE YA MSINGI MONIC WILAYA YA NGORONGORO KUSOMA KWA BIDII....

Posted on: November 9th, 2023

Na Elinipa Lupembe


Mkuu wa mkoa wa Arusha amewataka wanafunzi wa shule ya Msingi Monic, Wilaya ya Ngorongoroo,  kutia bidii kwenye masomo yao ili waweze kufaulu na kufikia ndoto zao, kwa kuwa serikali inategemea kupata watalamu wa kulitumikia Taifa hili kupitia wao.


Amesema hayo wakati akizungumza na wanafunzi wa shule hiyo, mara baada ya kukagua mradi wa ujenzi wa vyumba vya madarasa shuleni hapo, mradi uliotekelezwa na Serikali kupitia programu ya BOOST.


Mhe. Mongella amewaasa wanafunzi hao kusoma kwa bidii kwa kuwa serikali yao ya awamu ya sita inayoongozwa na Dkt. Samia Suluhu Hassan inawajali kwa kuwawekea mazingira bora na rafiki ya kujifunzia.


Amesema kuwa serikali imejenga madarasa mazuri  ili kila mtoto wa Sale aweze kusoma na kufika ndoto zake za kupata ujuzi na maarifa ya kulitumikia Taifa la Tanzania mara baada ya kuhitimu masomo yake ya shule.


"Serikali inawajengea madarasa mazuri ili msome vizuri, fanyani bidii, bibi yenu mama Samia anataka muwe watalamu wa kulitumikia Taifa lenu, anapostafu kazi ninyi ndio mjekuwa viongozi wa nchi hii, Rais atoke hapa shule ya Monic, msimuangushe".Amesema Mhe. Mongella


Hata hivyo wanafunzi hao wa Monic licha ya kumshukuru Mama Samia wameahidi kusoma kwa bidii na kufia ndoto zao za kuwa watalamu wa kulitumikia Taifa kama yalivyo malengo ya Serikali yao.


Dada Mkuu wa shule, Sinyati Saitabau amemshukuru Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuwajengea madarasa mazuri, yanapendeza ambayo kwa sasa wanasoma vizuri na kuahidi kuhamasisha wenzake kuongeza bidii kwenye masomo ili waweze kufaulu


"Tunamshukuru mama Samia, ametukumbuka wanafunzi wa Monic, madarasa ni mazuri sana yanapendeza na sisi tutasoma sana, kama kiongozi nitawahimiza wenzangu kuongeza bidii kwenye masomo na kufaulu vizuri" Amesema Sinyati.


Naye Mwalimu Mkuu wa shule hiyo amesema kuwa madarasa hayo ni muhimu shuleni hapo kwani yamepunguza msongamano wa wanafunzi darasani na kurahisisha tendo la kujifunza na kufundisha kwa walimu na wanafunzi.


Aidha amesema kuwa wao kama walimu wameridhishwa na utendaji wa serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Mhe. Dkt. Samia na wanaahidi kufanya kazi kwa weledi ya kuwafundisha wanafunzi ili kufikia malengo ya Serikali na wanafunzi kufikia ndoto zao.



Tangazo

  • TAZAMA MATOKEO YA MTIHANI WA MOCK MKOA DARASA LA SABA 1 July 06, 2023
  • MATOKEO YA MOCK MKOA DARASA LA SABA 2 July 07, 2023
  • TAZAMA MATOKEO YA MOCK MKOA KIDATO CHA NNE July 07, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONDA ASHUHUDIA UTIAJI SAINI UJENZI WA BARABARA YA ESO - LONGDON NA UKUMBI WA MIKUTANO ARUSHA.

    April 03, 2025
  • RC MAKONDA ATAKA KUPEWA MAJINA YA WATENDAJI WANAOCHOCHEA MIGOGORO YA KIJAMII.

    March 28, 2025
  • KAMPENI YA MSAADA WA KISHERIA NI MAONO NA MAELEKEZO YA RAIS SAMIA- WAZIRI NDUMBARO.

    March 28, 2025
  • OFISI YA MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI YAFANYIA KAZI MALALAMIKO WANANCHI WA MIANZINI ARUSHA.

    March 28, 2025
  • Angalia Zote

Video

UZINDUZI WA BARABARA YA WASO-SALE
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • SALARY SLIP
  • Taarifa ya Mapato
  • Taarifa za Shule (SIS)
  • Takwimu za Sekta ya Elimu (BEMIS)
  • Video

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Portal ya Watumishi
  • Takwimu
  • TANAPA

Watembeleaji

world map hits counter

Wasiliana Nasi

Mawaliliano mengine

   

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani
    • Maswali ya Mara kwa Mara

Hatimiliki ©2018 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Arusha. Haki Zote Zimehifadhiwa