• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Arusha Regional

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Mkoa
      • Chimbuko/Asili ya eneo
      • Orodha ya wakuu wa Mikoa
    • Dira na dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji Mali
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Wilaya
    • Arusha
      • Historia
      • Viongozi
    • Arumeru
      • Historia
      • Viongozi
    • Monduli
      • Historia
      • Viongozi
    • Karatu
      • Historia
      • Viongozi
    • Longido
      • Historia
      • Viongozi
    • Ngorongoro
      • Historia
      • Viongozi
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Arusha
    • Halmashauri ya Arusha
    • Halmashauri ya Meru
    • Halmashauri ya Monduli
    • Halmashauri ya Karatu
    • Halmashauri ya Longido
    • Halmashauri ya Ngorongoro
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo
    • Viwanda
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Ardhi
    • Utalii
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali
    • Habari
    • Matukio

SOMALIA MWANACHAMA MPYA NCHI ZA JUMUIYA YA AFRIKA MASHARIKI

Posted on: November 24th, 2023

 Na Elinipa Lupembe.


Wakuu wa Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, wameyakubali maombi ya Nchi ya Somalia, kuwa Mwanachama wa Nchi za Jumuyia hiyo ya Afrika Mashariki na kuifanya Jumuiya hiyo kuwa na Nchi 8, ikiwemo.Tanzania, Kenya, Uganda, Burundi, Rwanda, Sudan Kusini, Jamhuri ya Demokrasia ya Kongo, na Somalia


Maamuzi hayo, yalifanyika kwenye kikao cha Ndani na hatimaye, kuyaweka bayana, wakati wa kuhitimisha,  Mkutano wa 23 wa Kawaida wa Wakuu wa Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC), uliofanyika Mkoani Arusha, kwenye viwanja vya Hoteli ya Ngurdoto Mountain Lodge wilayani Arumeru.


Licha ya kuwa, Rais wa Somalia Mhe. Hassan Sheikh Mohamud,  alihudhuria Mkutano huo wa 23, kwa mara ya kwanza, na Nchi yake kukubaliwa kuwa mwanachama wa Jumuiya hiyo, huku Marais wa Jumuiya hiyo wakipata wasaa wa kumpongeza Rais huyo kwa niaba ya wananchi wa nchi hiyo, kwa kujiunga na kuwa mwanachama wa Umoja huo muhimu kwa manufaa na maendeleo ya wananchi wa nchi hizo.


Naye, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Dkt. Samia Suluhu Hassan, amempongeza Rais wa Somalia, kwa  kujiunga na Jumuiya hiyo pamoja na kushiriki mjadala wa mabadiliko ya tabia Nchi na Usalama wa Chakula, wenye lengo la kujiweka imara katika kukabiliana na changamoto zinazotokana na mabadiliko hayo bila kutegemea misaada kutoka nje ya Afrika.


"Tumefurahia nchi ya Somalia kujumuika nasi, kwa kuwa sisi ni ndugu moja, tunayo mengi zaidi tunayofanana kuliko tunayotofautiana" Amesema Mhe. Samia


Awali, katika mkutano huo, Rais wa Sudan Mhe. Salva Kiir  Mayardit, amekuwa Mwenyekiti wa Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, baaaya kupokea kijiti kutoka kwa Rais wa Burundi Mhe. Evariste Ndayishimiye, ambaye  amemalliza muda wake.


Mara baada ya kuchaguliwa, Mhe. Salva Kiiri, amekabidhiwa nyenzo za kufanyia kazi, kwa kipindi chote cha kuiongoza Jumuiya hiyo, nafasi ambayo inadumu kwa kipindi cha mwaka mmoja.


Mkutano huo wa siku mbili, ulihusisha Wakuu wa  Nchi za Wananchama wa Jumuiya za Afrika Mashariki,  licha ya mambo mengine yaliyojadiliwa, ulijikita katika kujadili kuhusu masuala ya Tabia Nchi na Usalama wa Chakula, ukiwa umebeba Kauli Mbiu ya "Kuharakisha ufufuaji wa uchumi kupitia hatua za hali ya hewa na kuimarisha usalama wa chakula kwa ajili ya kuboresha maisha" (Theme Accelerating Economic Recovery through Climate Action and enhancing Food Security for Improved Livelihoods), ukitanguliwa na vikao vya ndani tarehe 23 Novemba na kumalizika,  tarehe 24 Novemba, 2023.


#eastafricacommunity


Tangazo

  • TAZAMA MATOKEO YA MTIHANI WA MOCK MKOA DARASA LA SABA 1 July 06, 2023
  • MATOKEO YA MOCK MKOA DARASA LA SABA 2 July 07, 2023
  • TAZAMA MATOKEO YA MOCK MKOA KIDATO CHA NNE July 07, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONDA ASHUHUDIA UTIAJI SAINI UJENZI WA BARABARA YA ESO - LONGDON NA UKUMBI WA MIKUTANO ARUSHA.

    April 03, 2025
  • RC MAKONDA ATAKA KUPEWA MAJINA YA WATENDAJI WANAOCHOCHEA MIGOGORO YA KIJAMII.

    March 28, 2025
  • KAMPENI YA MSAADA WA KISHERIA NI MAONO NA MAELEKEZO YA RAIS SAMIA- WAZIRI NDUMBARO.

    March 28, 2025
  • OFISI YA MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI YAFANYIA KAZI MALALAMIKO WANANCHI WA MIANZINI ARUSHA.

    March 28, 2025
  • Angalia Zote

Video

UZINDUZI WA BARABARA YA WASO-SALE
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • SALARY SLIP
  • Taarifa ya Mapato
  • Taarifa za Shule (SIS)
  • Takwimu za Sekta ya Elimu (BEMIS)
  • Video

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Portal ya Watumishi
  • Takwimu
  • TANAPA

Watembeleaji

world map hits counter

Wasiliana Nasi

Mawaliliano mengine

   

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani
    • Maswali ya Mara kwa Mara

Hatimiliki ©2018 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Arusha. Haki Zote Zimehifadhiwa