• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Arusha Regional

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Mkoa
      • Chimbuko/Asili ya eneo
      • Orodha ya wakuu wa Mikoa
    • Dira na dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji Mali
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Wilaya
    • Arusha
      • Historia
      • Viongozi
    • Arumeru
      • Historia
      • Viongozi
    • Monduli
      • Historia
      • Viongozi
    • Karatu
      • Historia
      • Viongozi
    • Longido
      • Historia
      • Viongozi
    • Ngorongoro
      • Historia
      • Viongozi
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Arusha
    • Halmashauri ya Arusha
    • Halmashauri ya Meru
    • Halmashauri ya Monduli
    • Halmashauri ya Karatu
    • Halmashauri ya Longido
    • Halmashauri ya Ngorongoro
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo
    • Viwanda
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Ardhi
    • Utalii
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali
    • Habari
    • Matukio

TANZANIA NA KENYA NI NDUGU

Posted on: December 1st, 2018

Kituo cha forodha cha mpaka wa Namanga mkoani Arusha kinatarajia kukusanya mapato ya kiasi cha bilioni 53 kwa mwaka 2019.

Yamesemwa hayo na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli alipokuwa akifungua kituo cha pamoja cha forodha kati ya Tanzania na Kenya katika mpaka wa Namanga Arusha.

“Vituo hivi vya huduma ya pamoja vinasaidia kurahisisha usafiri, kukuza biashara na utalii na urahisi kwa wananchi wetu kuvuka mpakani mara  kwa mara.”

Amesema nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki zinachangamoto ya kuwa na vikwanzo vya kibiashara vinavyopeleka uchumi wa nchi hizi kudolola ukilinganisha na mabara mengine kama ya Amerika.

Kutokana na changamto hiyo nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki zikachukua uwamuzi wa kuanzisha vituo vya forodha vitakavyo saidia kukuza biashara kwa nchi husika.

Nae Rais wa Jamhuri ya Kenya Uhuru Kenyata amesema, kituo hicho kiwe chachu ya kuwasaidia wafanyabiashara wadogo kukuza biashara zao kwani wao ndio msingi wa uchumi katika nchi zetu.

Kenyata amesema ni wajibu wa watumishi wa kituo hicho kuwasaidia na kuwajali wafanyabiashara hao wadogo na wao wafanyabiashara wafuate sheria za nchi husika na biashara zao ziwe halali.

Amesema jukumu la serikali ni kuhakikisha wananchi wake wanafanya biashara kwa haki na uhuru bila ubuguzi wowote.

Gavana wa jimbo la Kajado Joseph Oleleku, alisema ili nchi hizi mbili ziweze kunufaika na fursa za biashara amekuwa akifanya mikutano ya mara kwa mara ili kuhakikisha wafanyabaishara wanapata haki zao na wanafanya biashara zao kwa uhuru.

Akitoa neno la ukaribisho mkuu wa Mkoa wa Arusha Mrisho Gambo amesema,Mkoa umeendelea kuhakikisha usalama wa mpaka huo unaimarika kwa kiasi kikubwa kwa kuongeza ulinzi wa kutumia mbwa.

Gambo amesema mbali na huduma nzuri iliyopo katika mpaka huo kuna changamoto ya ukosefu wa scanna kwa ajili ya ukaguzi wa magari makubwa, ukosefu wa huduma ya upimaji wa ubora wa bidhaa  zinazoingia na kutoka mpakani.

Magufuli yupo katika ziara ya siku 2 mkoani Arusha ambapo amefungua kituo cha pamoja cha forodha na ataweka jiwe la msingi katika mradi mkubwa wa maji katika jiji la Arusha na wilaya ya Arumeru.

Tangazo

  • TAZAMA MATOKEO YA MTIHANI WA MOCK MKOA DARASA LA SABA 1 July 06, 2023
  • MATOKEO YA MOCK MKOA DARASA LA SABA 2 July 07, 2023
  • TAZAMA MATOKEO YA MOCK MKOA KIDATO CHA NNE July 07, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONDA ASHUHUDIA UTIAJI SAINI UJENZI WA BARABARA YA ESO - LONGDON NA UKUMBI WA MIKUTANO ARUSHA.

    April 03, 2025
  • RC MAKONDA ATAKA KUPEWA MAJINA YA WATENDAJI WANAOCHOCHEA MIGOGORO YA KIJAMII.

    March 28, 2025
  • KAMPENI YA MSAADA WA KISHERIA NI MAONO NA MAELEKEZO YA RAIS SAMIA- WAZIRI NDUMBARO.

    March 28, 2025
  • OFISI YA MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI YAFANYIA KAZI MALALAMIKO WANANCHI WA MIANZINI ARUSHA.

    March 28, 2025
  • Angalia Zote

Video

UZINDUZI WA BARABARA YA WASO-SALE
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • SALARY SLIP
  • Taarifa ya Mapato
  • Taarifa za Shule (SIS)
  • Takwimu za Sekta ya Elimu (BEMIS)
  • Video

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Portal ya Watumishi
  • Takwimu
  • TANAPA

Watembeleaji

world map hits counter

Wasiliana Nasi

Mawaliliano mengine

   

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani
    • Maswali ya Mara kwa Mara

Hatimiliki ©2018 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Arusha. Haki Zote Zimehifadhiwa