• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Arusha Regional

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Mkoa
      • Chimbuko/Asili ya eneo
      • Orodha ya wakuu wa Mikoa
    • Dira na dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji Mali
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Wilaya
    • Arusha
      • Historia
      • Viongozi
    • Arumeru
      • Historia
      • Viongozi
    • Monduli
      • Historia
      • Viongozi
    • Karatu
      • Historia
      • Viongozi
    • Longido
      • Historia
      • Viongozi
    • Ngorongoro
      • Historia
      • Viongozi
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Arusha
    • Halmashauri ya Arusha
    • Halmashauri ya Meru
    • Halmashauri ya Monduli
    • Halmashauri ya Karatu
    • Halmashauri ya Longido
    • Halmashauri ya Ngorongoro
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo
    • Viwanda
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Ardhi
    • Utalii
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali
    • Habari
    • Matukio

*TANZANIA YAUNGA MKONO UAMUZI WA SADC; UVUNAJI MAJI KUDHIBITI MAFURIKO - WAZIRI MKUU MAJALIWA*...

Posted on: May 23rd, 2024

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema, Tanzania inaunga mkono uamuzi wa Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika (SADC) juu ya kuongeza mbinu za uvunaji wa maji, udhibiti wa mafuriko na miundombinu ya kuhifadhi maji hayo ili yatumike wakati wa ukame ama kiangazi kuzuia mafuriko msimu wa mvua nyingi.

“Tanzania inaunga mkono uamuzi huo na inasisitiza Sekretariet ya SADC kuongeza misaada kwa nchi wanachama katika ujenzi wa mabwawa ya kutunza maji ambayo yatatumika katika vipindi vya ukame na kiangazi pamoja na kuzuia mafuriko katika vipindi vya mvua,” amesema.

Waziri Mkuu amesema hayo leo (Jumatatu, Mei 20, 2024) wakati akizungumza kwa niaba ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwenye Mkutano wa Dharura wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa SADC kuhusu athari za mvua za El Nino. Ameshiriki mkutano huo kwa njia ya mitandao kutokea ofisini kwake Mlimwa, jijini Dodoma.

Maamuzi hayo yaliyopendekezwa kwenye kikao cha Mawaziri wa nchi wanachama wa jumuiya hiyo yalitaka ziongezwe mbinu za uvunaji wa maji, udhibiti wa mafuriko na miundombinu ya kuhifadhi maji kwa msaada kutoka kwa Sekretarieti ya SADC, Mashirika ya Uendelezaji Mabonde ya Mito (RBOs) na wadau wa maendeleo ili kuongeza nguvu ya kukabiliana na ukame ama mafuriko yanayosababishwa na hali ya hewa kwenye ukanda wa SADC.

Mapendekezo mengine yaliyotolewa ni kuboresha utendaji wa Usimamizi wa Rasilimali za Maji Jumuishi (IWRM); kufuatilia viwango vya maji na kutekeleza huduma za WASH; kuboresha usimamizi wa maji yanayohusisha nchi zaidi ya moja na ushirikiano wa kimataifa; kuhamasisha uhifadhi wa maji na kukuza matumizi ya maji machafu yaliyotibiwa na maji yaliyochujwa chumvi (desalination).

Akielezea kuhusu ujenzi wa mabwawa ya kutunzia maji ambayo yatatumika katika vipindi vya ukame na kiangazi pamoja na kuzuia mafuriko katika vipindi vya mvua, Waziri Mkuu aliwaeleza wajumbe wa mkutano huo kuwa Serikali ya Tanzania tayari imeandaa Mpango Mkakati wa Ujenzi Malambo 40 Nchini (rain water ponds) kuanzia Novemba 2023 hadi Julai 2024 ambao ni awamu ya kwanza.

Tangazo

  • TAZAMA MATOKEO YA MTIHANI WA MOCK MKOA DARASA LA SABA 1 July 06, 2023
  • MATOKEO YA MOCK MKOA DARASA LA SABA 2 July 07, 2023
  • TAZAMA MATOKEO YA MOCK MKOA KIDATO CHA NNE July 07, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONDA ASHUHUDIA UTIAJI SAINI UJENZI WA BARABARA YA ESO - LONGDON NA UKUMBI WA MIKUTANO ARUSHA.

    April 03, 2025
  • RC MAKONDA ATAKA KUPEWA MAJINA YA WATENDAJI WANAOCHOCHEA MIGOGORO YA KIJAMII.

    March 28, 2025
  • KAMPENI YA MSAADA WA KISHERIA NI MAONO NA MAELEKEZO YA RAIS SAMIA- WAZIRI NDUMBARO.

    March 28, 2025
  • OFISI YA MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI YAFANYIA KAZI MALALAMIKO WANANCHI WA MIANZINI ARUSHA.

    March 28, 2025
  • Angalia Zote

Video

UZINDUZI WA BARABARA YA WASO-SALE
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • SALARY SLIP
  • Taarifa ya Mapato
  • Taarifa za Shule (SIS)
  • Takwimu za Sekta ya Elimu (BEMIS)
  • Video

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Portal ya Watumishi
  • Takwimu
  • TANAPA

Watembeleaji

world map hits counter

Wasiliana Nasi

Mawaliliano mengine

   

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani
    • Maswali ya Mara kwa Mara

Hatimiliki ©2018 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Arusha. Haki Zote Zimehifadhiwa