• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Arusha Regional

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Mkoa
      • Chimbuko/Asili ya eneo
      • Orodha ya wakuu wa Mikoa
    • Dira na dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji Mali
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Wilaya
    • Arusha
      • Historia
      • Viongozi
    • Arumeru
      • Historia
      • Viongozi
    • Monduli
      • Historia
      • Viongozi
    • Karatu
      • Historia
      • Viongozi
    • Longido
      • Historia
      • Viongozi
    • Ngorongoro
      • Historia
      • Viongozi
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Arusha
    • Halmashauri ya Arusha
    • Halmashauri ya Meru
    • Halmashauri ya Monduli
    • Halmashauri ya Karatu
    • Halmashauri ya Longido
    • Halmashauri ya Ngorongoro
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo
    • Viwanda
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Ardhi
    • Utalii
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali
    • Habari
    • Matukio

TUMIENI ARDHI KWA MAENDELEO YENU-RC KIMANTA

Posted on: February 26th, 2021

Wanawake Wilayani Longido wametakiwa kutumia ardhi katika kuzalisha ili walete maendeleo katika familia zao na jamii kwa ujumla.

Yamesemwa hayo na Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe, Iddi Kimanta alipokuwa akigawa hati miliki za kimila kwa wanawake 233 kutoka Tarafa ya Engarenaibor katika Kijiji cha Mairowa Wilayani Longido.

“Niwapongeze sana wababa kwa kuridhia kutoa ardhi kwa ajili ya wamama, hiki ni kitendo cha ushujaa na faida ni kwa familia yote”.

Amesema Wilaya ya Longido imeweka historia mpya kwa kuwaruhusu wanawake kumiliki ardhi kitu ambacho hakikuwepo tokea mwanzo kutokana na mila na desturi za jamii ya Kimasai.

Kimanta amesema kupatikana kwa hati miliki hizo kuna toa fursa kwa wanawake kuweza kufanya shughuli mbalimbali za uzalishaji, ikiwemo kupata mikopo kutoka katika Halmashauri na Mabenki ili waweze kuwekeza zaidi katika miradi.

Amesisitiza kuwa kwa wanawake kumiliki ardhi kutasaidia kupunguza migogoro ya ardhi ambayo mingi ilikuwa inasababishwa na wamama wengi katika familia kushindwa kuwa na haki yakumiliki ardhi.

Aidha, Kimanta amesema serikali itashirikiana na Baraza la wanawake wafungaji (PWC) kuhakikisha wanawake katika jamii ya kimasai wanamiliki ardhi na kuwa na maamuzi ya kifamilia na hata jamii yao pia.

Nae katibu Tawala Wilaya ya Longido bwana Kamana Simba  akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya hiyo Mhe. Frank Mwausumbe amewataka wakinamama hao kutozifungia hati miliki hizo katika makabati, bali wakazitumie katika uzalishaji kwa maendeleo ya familia zao na jamii yote.

Mbunge wa jimbo la Longido Mhe. Steven Kiluswa amewataka wakinamama hao waliopewa hati miliki za ardhi kutoenda kuanzisha mafarakano katika familia zao.

Amewahasa pindi wanapotaka kuuza ardhi wawashirikishe waume zao au Watoto, wasiuze kimya kimya kwani ndio chanzo cha migogoro mingi ya ardhi katika jamii hiyo ya Kimasai.

Mashaka Mtatilo ni afisa ardhi kutoka halmashauri ya Longido amesema, mpaka sasa jumla ya vijiji 38 vimeshapimwa ardhi kati ya vijiji 49 na zoezi la upimaji linaendelea katika vijiji hivyo vilivyosalia.

Baraza la wanawake wafugaji limekuwa likitoa mchango mkubwa sana katika kuwainua wanawake wa jamii yakifugaji katika nyanja mbalimbali ikiwemo Elimu na Uchumi hasa katika wilaya hiyo ya Longido.

Tangazo

  • TAZAMA MATOKEO YA MTIHANI WA MOCK MKOA DARASA LA SABA 1 July 06, 2023
  • MATOKEO YA MOCK MKOA DARASA LA SABA 2 July 07, 2023
  • TAZAMA MATOKEO YA MOCK MKOA KIDATO CHA NNE July 07, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONDA ASHUHUDIA UTIAJI SAINI UJENZI WA BARABARA YA ESO - LONGDON NA UKUMBI WA MIKUTANO ARUSHA.

    April 03, 2025
  • RC MAKONDA ATAKA KUPEWA MAJINA YA WATENDAJI WANAOCHOCHEA MIGOGORO YA KIJAMII.

    March 28, 2025
  • KAMPENI YA MSAADA WA KISHERIA NI MAONO NA MAELEKEZO YA RAIS SAMIA- WAZIRI NDUMBARO.

    March 28, 2025
  • OFISI YA MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI YAFANYIA KAZI MALALAMIKO WANANCHI WA MIANZINI ARUSHA.

    March 28, 2025
  • Angalia Zote

Video

UZINDUZI WA BARABARA YA WASO-SALE
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • SALARY SLIP
  • Taarifa ya Mapato
  • Taarifa za Shule (SIS)
  • Takwimu za Sekta ya Elimu (BEMIS)
  • Video

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Portal ya Watumishi
  • Takwimu
  • TANAPA

Watembeleaji

world map hits counter

Wasiliana Nasi

Mawaliliano mengine

   

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani
    • Maswali ya Mara kwa Mara

Hatimiliki ©2018 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Arusha. Haki Zote Zimehifadhiwa