• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Arusha Regional

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Mkoa
      • Chimbuko/Asili ya eneo
      • Orodha ya wakuu wa Mikoa
    • Dira na dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji Mali
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Wilaya
    • Arusha
      • Historia
      • Viongozi
    • Arumeru
      • Historia
      • Viongozi
    • Monduli
      • Historia
      • Viongozi
    • Karatu
      • Historia
      • Viongozi
    • Longido
      • Historia
      • Viongozi
    • Ngorongoro
      • Historia
      • Viongozi
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Arusha
    • Halmashauri ya Arusha
    • Halmashauri ya Meru
    • Halmashauri ya Monduli
    • Halmashauri ya Karatu
    • Halmashauri ya Longido
    • Halmashauri ya Ngorongoro
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo
    • Viwanda
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Ardhi
    • Utalii
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali
    • Habari
    • Matukio

WALIOKOSA MAKAZI KATESHI, SERIKALI YAJIPANGA KUWAPA MAKAZI YA KUDUMU...

Posted on: December 8th, 2023

Na Elinipa Lupembe


Serikali ya awamu ya sita, imejipanga kuzipa makazi ya kudumu kaya zilizokosa makazi  Kateshi, kufuatia maafa yaliyotokana na kumeguka sehemu ya mlima Hanang'  kusababisha uharibifu wa mali na maisha ya watu


Ahadi hiyo, imetolewa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, alipokuwa akizungumza na maelfu ya wakazi wa Kateshi, kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye  viwanja vya shule ya Msingi Kateshi.


Katika Mkutano huo, Mhe. Rais,  alitoa salama za pole kwa  watanzania hususani wakazi wa Kateshi, walipoteza ndugu, jamaa na marafiki, majeruhi pamoja na wale waliokosa amakazi.


Mheshimiwa Rais, amesema kuwa zipo kaya takribani  440 zilizokosa makazi na  kuthibitisna kuwa, Serikali imejipanga kuandaa eneo ambalo wataandaliwa makazi ya kudumu.


"Nimeagiza watalamu kufanya taarifa za uchunguzi wa kina, zinazohusu watu, mali na maeneo yote yaliyoathiri na kutafuta eneo, na bahati nzuri tumeshapata eneo ambalo watalamu litarasmishwa na Serikali ikifanya mpango wa kuwaandalia makazi ya kudumu ili waweze kuondoka kwenye makamazi ya muda" Amesema


Hata hivyo Mhe. Rais licha yakuwaapa pole wakazi wa Hana ng, amewashukuru na kuwapongeza kwa nidhamu na utulivu wa hali ya juu, walionyesha kipindi chote tangu maafa yaliopotekea na  kuendelea kuomboleza kwa amani huku wakifuata maelekezo, waaliyopewa na viongozi wao wa dini, mila na Serikali.


Aidha, amewashuku watanzania wote makampuni, taasisi, mashirika, mikoa jirani, waliyotekeza waliowakimbilia wanakatesh nankutoa misaada ya hali na mali, ikiwemo vyakula, magodoro, mablanketi na huduma zote za msingi ambazo zilihitajika kwa haraka, na kuthibitisha kuwa, huo ndio kitendo hicho kimeonesha uzalendo, umoja na upendo miongoni mwa watanzania.


Akiwasiliisha taarifa ya maafa hayo, Waziri wa Nchi Ofisi ya  Waziri Mkuu, Sera, Bunge na Uratibu, Mhe. Jenista Mhagama, amesema kuwa, maafa hayo yamesababisha vifo vya watu 76 majeruhi 117, kaya 1,150 zenye watu 5,600 zikiathitika huku watu 440 zilizopoteza makazi na kuhifadhiwa kwenye kambi maalum za shule ya sekondari Kateshi na Ganana na shule ya msingi Genabi.


"Kwa maelekezo yako Mhe. Rais, serikali iligharamia mazishi ya marehemu 76 kwa kushirikiana na familia zao, na kutoa huduma zote ikiwemo malazi na chakula kwa kaya 1,150 zilizokosa makazi pamoja na kuwatibu majeruhi 117 waliolazwa kwenye vituo vya afya Kateshi na Babati"Amefafanua Mhe. Jenista


Waziri Mkuu, Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa, amemshukuru Mheshimiwa Rais, kwa kutoa maelekezo ya haraka katika kukabiliana na Maafa hayo, maagizo ambayo yametekeelezwa na watalamu wake, na kuhakikisha wananchi wa Katesh, wanapata huduma stahiki licha ya kupoteza jamaa na mali zao.


"Ninakuaahidi watalamu wa sekta mbalimbali wataendelea kuweka kambi hapa Katesh, mpaka hali ya itakapokuwa shwari na kuhakikisha wananchi wanarejea na kuendelea na shughuli zao za kawaida, tunayo akiba ya chakula ya kutosha kuwahudumia wahanga na watalamu kwa muda wa mwezi mmoja" Waziri Mkuu.


Tangazo

  • TAZAMA MATOKEO YA MTIHANI WA MOCK MKOA DARASA LA SABA 1 July 06, 2023
  • MATOKEO YA MOCK MKOA DARASA LA SABA 2 July 07, 2023
  • TAZAMA MATOKEO YA MOCK MKOA KIDATO CHA NNE July 07, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONDA ASHUHUDIA UTIAJI SAINI UJENZI WA BARABARA YA ESO - LONGDON NA UKUMBI WA MIKUTANO ARUSHA.

    April 03, 2025
  • RC MAKONDA ATAKA KUPEWA MAJINA YA WATENDAJI WANAOCHOCHEA MIGOGORO YA KIJAMII.

    March 28, 2025
  • KAMPENI YA MSAADA WA KISHERIA NI MAONO NA MAELEKEZO YA RAIS SAMIA- WAZIRI NDUMBARO.

    March 28, 2025
  • OFISI YA MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI YAFANYIA KAZI MALALAMIKO WANANCHI WA MIANZINI ARUSHA.

    March 28, 2025
  • Angalia Zote

Video

UZINDUZI WA BARABARA YA WASO-SALE
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • SALARY SLIP
  • Taarifa ya Mapato
  • Taarifa za Shule (SIS)
  • Takwimu za Sekta ya Elimu (BEMIS)
  • Video

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Portal ya Watumishi
  • Takwimu
  • TANAPA

Watembeleaji

world map hits counter

Wasiliana Nasi

Mawaliliano mengine

   

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani
    • Maswali ya Mara kwa Mara

Hatimiliki ©2018 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Arusha. Haki Zote Zimehifadhiwa