• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Arusha Regional

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Mkoa
      • Chimbuko/Asili ya eneo
      • Orodha ya wakuu wa Mikoa
    • Dira na dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji Mali
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Wilaya
    • Arusha
      • Historia
      • Viongozi
    • Arumeru
      • Historia
      • Viongozi
    • Monduli
      • Historia
      • Viongozi
    • Karatu
      • Historia
      • Viongozi
    • Longido
      • Historia
      • Viongozi
    • Ngorongoro
      • Historia
      • Viongozi
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Arusha
    • Halmashauri ya Arusha
    • Halmashauri ya Meru
    • Halmashauri ya Monduli
    • Halmashauri ya Karatu
    • Halmashauri ya Longido
    • Halmashauri ya Ngorongoro
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo
    • Viwanda
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Ardhi
    • Utalii
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali
    • Habari
    • Matukio

WASICHANA SEKONDARI MRINGA WAMSHUKURU MAMA SAMIA KWA KUWAJALI WASICHANA NCHINI..

Posted on: November 9th, 2023


Na Elinipa Lupembe


Wanafunzi wasichana shule ya sekondari Mringa wamemshukuru mama Samia, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuwajali na kuwapa kipaumbele kwa kuweka mazingira rafiki ya upatikanaji wa elimu kwa wasichana nchini.


Wakizungumza na mwandishi wa habari hizi shuleni kwao, wamethibitisha kuwa serikali ya awamu ya sita licha ya kuendelea kuboresha mazingira ya elimu nchini lakini imeenda mbali zaidi kwa kujenga miundombinu ya mabweni ya wasichana shuleni, inayowapa fursa watoto wa kike kusoma katika mazingira rafiki na wezeshi.


Simalo Mayenga mwanafunzi wa kidato cha 6, amesema kuwa ujenzi wa mabweni ya wasichana shuleni kwao, unadhihirisha namna Rais mama Samia anavyo wajali na kutoa kipaumbele kwa  wasichana  nchini ili waweze kupata elimu kwenye mazingira mazuri na wezeshi.


"Ujenzi wa mabweni unatuwezesha wasichana kusoma vizuri na kufikia ndoto zetu, ndoto ambazo zilizimwa kwa wasichana wengi kwa kukatishwa masomo kutokana na changamoto mbalimbali za kusoma shule za kutwa, kwa sasa wasichana wamehakikishiwa usalama wao katika safari yao ya masomo " Amesema Asimwe


Britney Baraka, anayesoma ya tahususi ya HGL, amesema kuwa ujenzi wa mabweni mawili shuleni hapo, unatoa fursa kwa wasichana kusoma vizuri na kwa uhuru huku wakiepukana na hatari zinazowapata wasichana wengi wanasoma shule za kutwa.


Naye Asimwe Garasian anayesoma tahususi ya  EGM, amethibitisha kuwa, wanafunzi wa kutwa hukumbana na changamoto nyingi za kijamii njiani, uwepo wa mabweni ya wasichana unatoa fursa kuepukana nazo kutokana na kuishi kwenye mazingira rafiki na kusoma kwa usalama bila kubughudhiwa.


Awali serikali ya awamu ya sita kupitia programu ya kuboresha miundombinu ya shule za sekondari (SEQUIP), imetoa shilingi milioni 360 kwa ajili ya ujenzi wa mabweni mapya mawili na ukarabati wa mabweni manne ya zamani.


Makamu mkuu wa shule ya sekondari Mringa, Mwl. Kleruu Zakaria Sumaye, amesema kuwa, shilingi milioni 260 zimejenga mabweni mapya mawili yenye uwezo wa kulaza wanafunzi 160 na 80 kwa kila bweni na milioni 100 zimetumika kukarabati mabweni manne yaliyojengwa zaidi ya miaka 70 iliyopita.


Tangazo

  • TAZAMA MATOKEO YA MTIHANI WA MOCK MKOA DARASA LA SABA 1 July 06, 2023
  • MATOKEO YA MOCK MKOA DARASA LA SABA 2 July 07, 2023
  • TAZAMA MATOKEO YA MOCK MKOA KIDATO CHA NNE July 07, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONDA ASHUHUDIA UTIAJI SAINI UJENZI WA BARABARA YA ESO - LONGDON NA UKUMBI WA MIKUTANO ARUSHA.

    April 03, 2025
  • RC MAKONDA ATAKA KUPEWA MAJINA YA WATENDAJI WANAOCHOCHEA MIGOGORO YA KIJAMII.

    March 28, 2025
  • KAMPENI YA MSAADA WA KISHERIA NI MAONO NA MAELEKEZO YA RAIS SAMIA- WAZIRI NDUMBARO.

    March 28, 2025
  • OFISI YA MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI YAFANYIA KAZI MALALAMIKO WANANCHI WA MIANZINI ARUSHA.

    March 28, 2025
  • Angalia Zote

Video

UZINDUZI WA BARABARA YA WASO-SALE
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • SALARY SLIP
  • Taarifa ya Mapato
  • Taarifa za Shule (SIS)
  • Takwimu za Sekta ya Elimu (BEMIS)
  • Video

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Portal ya Watumishi
  • Takwimu
  • TANAPA

Watembeleaji

world map hits counter

Wasiliana Nasi

Mawaliliano mengine

   

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani
    • Maswali ya Mara kwa Mara

Hatimiliki ©2018 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Arusha. Haki Zote Zimehifadhiwa