• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Arusha Regional

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Mkoa
      • Chimbuko/Asili ya eneo
      • Orodha ya wakuu wa Mikoa
    • Dira na dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji Mali
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Wilaya
    • Arusha
      • Historia
      • Viongozi
    • Arumeru
      • Historia
      • Viongozi
    • Monduli
      • Historia
      • Viongozi
    • Karatu
      • Historia
      • Viongozi
    • Longido
      • Historia
      • Viongozi
    • Ngorongoro
      • Historia
      • Viongozi
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Arusha
    • Halmashauri ya Arusha
    • Halmashauri ya Meru
    • Halmashauri ya Monduli
    • Halmashauri ya Karatu
    • Halmashauri ya Longido
    • Halmashauri ya Ngorongoro
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo
    • Viwanda
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Ardhi
    • Utalii
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali
    • Habari
    • Matukio

WATENDAJI WA KATA WAAGIZWA KUSIMAMIA VEMA UTEKELEZAJI WA ILANI YA CCM

Posted on: February 29th, 2024


Maofisa Watendaji wa Kata Mkoani Arusha, wametakiwa kusimamia vema utekelezaji wa Ilani ya CCM kwa kuhakikisha shughuli zote za maendeleo zinasimamiwa ikiwa ni pamoja na usimamizi wa utekelezaji wa miradi ya maendeleo pamoja  na kufanyika kwa vikao na mikutano yote ya kisheria.


Rai hiyo imetolewa wakati wa kikao cha majumuisho, ya ziara ya kawaida ya ukaguzi wa miradi ya maendeleo wilayani Longido, ikiwa ni ufuatiliaji wa utekelezaji wa Ilani ya Chama, iliyofanywa na Kamati ya  Siasa Mkoa wa Arusha.


Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa  wa Arusha Thomas Loy Ole Sabaya, 

amesisitiza kuwa moja ya jukumu la Maofisa Watendaji hao ni kusimamia miradi yote ya maendeleo inayofanyika katika maeneo yao, ikiwa ni pamoja kushirikisha wananchi kwa kupitia vikao na mikutano ya kisheria ili wananchi wafahamu  mambo yanaeyofanywa nra Serikiali ambayo ndio utekelezajiwa Ilani ya CCM.


Komredi Sabaya amesema kuwa, endapo Maofisa Watendaji watatekeleza majukumu yao na kutumiamia njia shirikishi ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo kwenye maeneo yao, watafikia malengo ya Serikali.


"Wananchi wanatakiwa kufahamu, kiasi cha fedha za miradi zilizoletwa na Serikali katika maeneo yao, zinatekeleza miradi gani, muda wa utekelezaji pamoja na kushiriki hatua zote za utelezaji na mwisho kuwasomea taarifa za mapato na matumizi kwa kila robo kupitia Wenyeviti na Watendaji wa vijiji". Amesema Sabaya


Hata hiyo, amemuagiza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Longido, Stephen Ulaya, kufanya msawazisho wa walimu katika shule zote, ili kuwe na uwiano wa walimu na wanafunzi unaoendana na idadi ya shule, hali itakayosaidia shule zote kuwa na walimu watakaowezesha wanafunzi kufundishwa masomo yote.


Katika kikao hicho, Diwani wa Kata ya Matale Lengai ole Nini, amemwomba Mwenyekiti huyo, kuwasaidia kupata walimu sita ili kuwa ni mbadala ya walimu waliohama mfululizo na kuwaacha  katika kata hiyo na kusababisha wanafunzi kukosa baadhi ya masomo.


"Walimu sita wamehama katika shule ya msingi Matala, wanafunzi wamebaki hawana walimu hatuwatendei haki, tunaomba walimu wengine mbadala ili kuziba pengo hilo". Amesisitiza Mhe.Ole Nini.


Naye Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mhe. John V.K Mongella ameahidi kuchukulia kwa uzito unaostahili hoja ya walimu na kuifanyia kazi huku akikiri kuwa bado kuna upungufu wa walimu kutokana na ongezeko kubwa la idadi ya shule mpya na kufafanua kuwa licha ya kuwa uhamisho ni haki ya mtumishi ni lazima Maofisa Elimu kufanya kwa umakini mkubwa ili kuhakikikisha shule haikosi walimu.


Mhe. Mongella amemsisitiza Mkuu wa Idara ya Elimu, kupeleka walimu wengine mbadala kweye shule hiyo ili kuziba pengo la walimu hao waliohama kabla ya kufikia tarehe 15, Machi  mwaka huu.


Awali Kamati ya siasa imefanya ziara ya siku mbili ya kukagua hali ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo na kuridhishwa na utekelezaji wa Ilani ya CCM ya mwaka 2020 -2025, uliofanyika kwa vitendo kama Mhe. Rais alivyoahidi kuitekeza mara baada ya kuingia madarakani.


Tangazo

  • TAZAMA MATOKEO YA MTIHANI WA MOCK MKOA DARASA LA SABA 1 July 06, 2023
  • MATOKEO YA MOCK MKOA DARASA LA SABA 2 July 07, 2023
  • TAZAMA MATOKEO YA MOCK MKOA KIDATO CHA NNE July 07, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONDA ASHUHUDIA UTIAJI SAINI UJENZI WA BARABARA YA ESO - LONGDON NA UKUMBI WA MIKUTANO ARUSHA.

    April 03, 2025
  • RC MAKONDA ATAKA KUPEWA MAJINA YA WATENDAJI WANAOCHOCHEA MIGOGORO YA KIJAMII.

    March 28, 2025
  • KAMPENI YA MSAADA WA KISHERIA NI MAONO NA MAELEKEZO YA RAIS SAMIA- WAZIRI NDUMBARO.

    March 28, 2025
  • OFISI YA MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI YAFANYIA KAZI MALALAMIKO WANANCHI WA MIANZINI ARUSHA.

    March 28, 2025
  • Angalia Zote

Video

UZINDUZI WA BARABARA YA WASO-SALE
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • SALARY SLIP
  • Taarifa ya Mapato
  • Taarifa za Shule (SIS)
  • Takwimu za Sekta ya Elimu (BEMIS)
  • Video

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Portal ya Watumishi
  • Takwimu
  • TANAPA

Watembeleaji

world map hits counter

Wasiliana Nasi

Mawaliliano mengine

   

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani
    • Maswali ya Mara kwa Mara

Hatimiliki ©2018 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Arusha. Haki Zote Zimehifadhiwa