• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Arusha Regional

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Mkoa
      • Chimbuko/Asili ya eneo
      • Orodha ya wakuu wa Mikoa
    • Dira na dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji Mali
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Wilaya
    • Arusha
      • Historia
      • Viongozi
    • Arumeru
      • Historia
      • Viongozi
    • Monduli
      • Historia
      • Viongozi
    • Karatu
      • Historia
      • Viongozi
    • Longido
      • Historia
      • Viongozi
    • Ngorongoro
      • Historia
      • Viongozi
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Arusha
    • Halmashauri ya Arusha
    • Halmashauri ya Meru
    • Halmashauri ya Monduli
    • Halmashauri ya Karatu
    • Halmashauri ya Longido
    • Halmashauri ya Ngorongoro
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo
    • Viwanda
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Ardhi
    • Utalii
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali
    • Habari
    • Matukio

WAZAZI HAKIKISHENI WATOTO WANAPATA CHANJO YA MIEZI 18

Posted on: October 15th, 2019

Wazazi wenye watoto chini ya miaka mitano watakiwa kuhakikisha watoto wao wanapata chanjo zote ili waweze kupata kinga kamili ya miili yao na kuwajengea afya bora.

Yamesemwa hayo na mratibu wa chanjo Mkoa wa Arusha bwana Azizi Sheshe alipokuwa akitoa mafunzo kwa waandishi wa habari juu ya kampeni shirikishi ya Surua,Rubella na Polio itakayofanyika nchi nzima mapema Octoba.

Amesema kwa mkoa wa Arusha utoaji wa chanjo upo katika hali nzuri japo changamoto kubwa ipo katika utoaji chanjo ya watoto wenye umri wa miezi 18, ambapo wazazi wengi wamekuwa wakiwapeleka  watoto wao katika chanjo ya kwanza ya miezi 9 tu.

“Wazazi wengi wamekuwa wakipuuzia chanjo ya pili ya miezi 18 kwa watoto na hali hii imepelekea watoto wengi kutokuwa na kinga kamili ya miili yao”.

Kutokana na changamoto hii ndio maana serikali imeamua kufanya kampeni hii nchi nzima ili kuhamasisha watoto wote waweze kupatiwa chanjo ya Surua, Rubella na Polio ili kuwaongezea kinga kamili katika miili yao.

Amesisitiza kuwa katika kampeni hii ambayo hata katika mkoa wa Arusha itafanyika na walengwa ni watoto wote walio chini ya miaka mitano na watapatiwa chanjo hiyo katika vituo mbalimbali vilivyoainishwa kwenye makazi ya watu.

Amewataka wazazi wote kuhakikisha watoto wao walio chini ya miaka mitano wanapatiwa chanjo hiyo hata kama alishapata zote mwanzo anaruhusiwa kurudia ili kumuweka katika nafasi nzuri zaidi ya kuongeza kinga ya mwili.

Amesema ugonjwa wa Surua na Rubella yanaenezwa kawa njia ya hewa hasa kwa kukohoa au kupiga chafya na ni magonjwa yanayoenea kwa kasi sana,wakati ugonjwa wa Polio unaenezwa kwa njia  ya ulaji chakula kichafu au maji yaliyochafuliwa.

Bwana Sheshe  amesema adhari za ugonjwa wa  Surua kwa mtoto ni; masikio kutoa usaha, kupata vidonda vya macho,Nimonia, Utapiamlo, kuvimba ubongo na hata kupelekea kifo na Rubella madhara yake kwa mtoto ni kupata mtoto wa jicho, matatizo ya Moyo, Kutosikia vizuri, mtindio wa ubongo na matatizo ya ukuaji wa mwili.

Hivyo amewasisitiza wazazi wote wawapeleke watoto wao katika vituo vya kupatiwa chanjo ili kuwaongezea kinga ya mwili watoto wao na kuwaepusha na magonjwa mbalimbali yanayoweza kuwapata.

Dokta Thomas Lyimo mwakilishi kutoka UNICEF,amesema taasis yake inashirikiana vyema na serikali kwa kuhakikisha chanjo zinapatikana nchini kwa wingi na kwa wakati na amewataka wananchi wa mkoa wa Arusha kujitokeza kwa wingi kuwapatia chanjo watoto wao.

Kampeni shirikishi ya Surua na Rubella kwa Mkoa wa Arusha itaanza rasmi Octoba 17 hadi Octoba 21 katika vituo mbalimbali vilivyoainishwa na chanjo hiyo itatolewa bure na kwa mfumo wa sindano,hivyo wazazi wanatakiwa kuhakikisha watoto wao wenye umri chini ya miaka mitano wanapatiwa chanjo hiyo.

Tangazo

  • TAZAMA MATOKEO YA MTIHANI WA MOCK MKOA DARASA LA SABA 1 July 06, 2023
  • MATOKEO YA MOCK MKOA DARASA LA SABA 2 July 07, 2023
  • TAZAMA MATOKEO YA MOCK MKOA KIDATO CHA NNE July 07, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONDA ASHUHUDIA UTIAJI SAINI UJENZI WA BARABARA YA ESO - LONGDON NA UKUMBI WA MIKUTANO ARUSHA.

    April 03, 2025
  • RC MAKONDA ATAKA KUPEWA MAJINA YA WATENDAJI WANAOCHOCHEA MIGOGORO YA KIJAMII.

    March 28, 2025
  • KAMPENI YA MSAADA WA KISHERIA NI MAONO NA MAELEKEZO YA RAIS SAMIA- WAZIRI NDUMBARO.

    March 28, 2025
  • OFISI YA MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI YAFANYIA KAZI MALALAMIKO WANANCHI WA MIANZINI ARUSHA.

    March 28, 2025
  • Angalia Zote

Video

UZINDUZI WA BARABARA YA WASO-SALE
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • SALARY SLIP
  • Taarifa ya Mapato
  • Taarifa za Shule (SIS)
  • Takwimu za Sekta ya Elimu (BEMIS)
  • Video

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Portal ya Watumishi
  • Takwimu
  • TANAPA

Watembeleaji

world map hits counter

Wasiliana Nasi

Mawaliliano mengine

   

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani
    • Maswali ya Mara kwa Mara

Hatimiliki ©2018 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Arusha. Haki Zote Zimehifadhiwa