• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Arusha Regional

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Mkoa
      • Chimbuko/Asili ya eneo
      • Orodha ya wakuu wa Mikoa
    • Dira na dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji Mali
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Wilaya
    • Arusha
      • Historia
      • Viongozi
    • Arumeru
      • Historia
      • Viongozi
    • Monduli
      • Historia
      • Viongozi
    • Karatu
      • Historia
      • Viongozi
    • Longido
      • Historia
      • Viongozi
    • Ngorongoro
      • Historia
      • Viongozi
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Arusha
    • Halmashauri ya Arusha
    • Halmashauri ya Meru
    • Halmashauri ya Monduli
    • Halmashauri ya Karatu
    • Halmashauri ya Longido
    • Halmashauri ya Ngorongoro
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo
    • Viwanda
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Ardhi
    • Utalii
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali
    • Habari
    • Matukio

WAZAZI NA WALEZI ACHENI DHANA POTOFU JUU YA CHANJO

Posted on: October 18th, 2019

Wazazi na walezi wametakiwa kuachana na dhana potofu, badala yake, kuwapeleka watoto wenye umri wa miezi tisa mpaka miaka mitano, kupata chanjo dhidi ya ugonjwa wa Polio, Surua-Rubela kwa kuwa chanjo hizo zinaokoa maisha ya watoto pamoja na kuokoa gharama kubwa ,ambazo familia na taifa ingezitumia kwa kutibu magonjwa yanayoweza kuzuilika kwa kinga chanjo.

Akizungumza wakati wa uzinduzi wa Kampeni ya kitaifa ya Chanjo kimkoa, uzinduzi uliofanyika, kwenye kituo cha Afya cha Nduruma, Halmashauri ya Arusha, Katibu Tawala Mkoa wa Arusha, Richard Kwitega, amesema kuwa, lengo la kampeni ya chanjo kitaifa ni kutokomeza maradhi na kupunguza vifo vya watoto, pamoja na kuokoa gharama za kubwa za matibabu kwa magonjwa yanayoweza kuzuilika kupitia chanjo.

Katibu Tawala huyo, ameendelea kufafanua kuwa, tafiti zinaonesha kuwa, hadi kufikia mwaka 2019, magonjwa yanayokingika kwa chanjo yameendelea kuongezeka, kutoka magonjwa manne mpaka kufikia magonjwa 13, hivyo ni vyema kuchukua tahadhari na kuwataka wazazi kuhakikisha watoto wamepata chanjo zote muhimu, sambamba na kuwaongezea kinga zaidi, wakati zoezi la chanjo kitaifa linapojitokeza kama sasa.

Hata hivyo Katibu Tawala huyo, amesema kuwa, licha ya changamoto za umbali wa vituo vya kutolea huduma za afya, bado halmshauri zinaendelea kutoa huduma za mikoba kwa kuwafuata wananchi kokote walipo, huku Serikali ya awamu ya tano ikiwekeza fedha nyingi kwenye ujenzi wa vituo vya afya nchini, ili kuhakikisha wananchi wanapata huduma muhimu za afya ndani ya maeneo yao wanayoishi .

Awali, Katibu Tawala wilaya ya Arumeru, mwalimu James Nchembe, amesisitiza kuwa, chanjo hizo zinatolewa bure, na  zinatolewa kwenye vituo vyote vya kutolea huduma za afya ndani ya wilaya hiyo, hivyo ni vema kila mzazi kutenga saa chache kumpeleka mtoto wake kupata chanjo hizo. 

Naye Mkurugenzi Mtendaji, Halmashauri ya Arusha, Alvera Ndabagoye, ameisisitiza kuwa, ubora wa chanjo hizo, umethibitishwa kwa viwango vya kimataifa, hivyo ni vyema wazazi na walezi kupuuzia maneno ya uzushi dhidi ya chanjo hizo, na kuwapeleka watoto wa umri huo kupata chanjo hizo muhimu.

Ameongeza kuwa serikali inafanya kampeni ya kitaifa ya chanjo za Polio na Surua-Rubela, ikiwa na mkakati wa kuwa na taifa lenye watoto wasiosumbuliwa na maradhi, ikiwemo matatizo ya moyo, mtindio wa ubongo, upofu wala wenye kupooza viuno vya mwili.

Katika hali isiyotarajiwa mamia ya wazazi na walezi wamejitokeza kwa wingi, kwenye kituo cha Afya Nduruma, wakiwa wamembatana na watoto wao wenye umri wa kuanzia miezi 9 Hadi miaka 5, ili kupata chanjo hizo, huku wengi wao wakiipongeza serikali ya awamu ya tano, kwa kujali afya za wananchi wake, hasa waishio vijijini kama wao.

Leila Mohammed mkazi wa Kijiji cha Nduruma Kati, ameishukuru Serikali kwa kuleta chanjo hizo muhimu kwa watoto wao, na kuongeza kuwa Serikali imewapa elimu ya kutosha juu ya umuhimu wa chanjo hizo, jambo lililosababisha wazazi hao, kujitokeza kwa wingi kuwaleta watoto wao.

"Tumeelimishwa vya kutosha, umuhimu wa chanjo hizi, chanjo zinazuia magonjwa ya moyo, macho, ulemavu wa viungo na mtindio wa ubongo, imetulazimu kuwaleta watoto wetu, kwani hakuna mzazi anayependa mtoto wake apate matatizo" amesema Leila.

Mkoa wa Arusha umezindua rasmi kampeni ya utoaji chanjo ya Surua,Rubella na Polia kwa watoto kuanzia miezi 9 hado miaka mitano na kampeni hii itadumu kwa siku 5 kuanzia Octoba 17 hadi Octoba 21.

Tangazo

  • TAZAMA MATOKEO YA MTIHANI WA MOCK MKOA DARASA LA SABA 1 July 06, 2023
  • MATOKEO YA MOCK MKOA DARASA LA SABA 2 July 07, 2023
  • TAZAMA MATOKEO YA MOCK MKOA KIDATO CHA NNE July 07, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONDA ASHUHUDIA UTIAJI SAINI UJENZI WA BARABARA YA ESO - LONGDON NA UKUMBI WA MIKUTANO ARUSHA.

    April 03, 2025
  • RC MAKONDA ATAKA KUPEWA MAJINA YA WATENDAJI WANAOCHOCHEA MIGOGORO YA KIJAMII.

    March 28, 2025
  • KAMPENI YA MSAADA WA KISHERIA NI MAONO NA MAELEKEZO YA RAIS SAMIA- WAZIRI NDUMBARO.

    March 28, 2025
  • OFISI YA MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI YAFANYIA KAZI MALALAMIKO WANANCHI WA MIANZINI ARUSHA.

    March 28, 2025
  • Angalia Zote

Video

UZINDUZI WA BARABARA YA WASO-SALE
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • SALARY SLIP
  • Taarifa ya Mapato
  • Taarifa za Shule (SIS)
  • Takwimu za Sekta ya Elimu (BEMIS)
  • Video

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Portal ya Watumishi
  • Takwimu
  • TANAPA

Watembeleaji

world map hits counter

Wasiliana Nasi

Mawaliliano mengine

   

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani
    • Maswali ya Mara kwa Mara

Hatimiliki ©2018 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Arusha. Haki Zote Zimehifadhiwa