• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Arusha Regional

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Mkoa
      • Chimbuko/Asili ya eneo
      • Orodha ya wakuu wa Mikoa
    • Dira na dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji Mali
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Wilaya
    • Arusha
      • Historia
      • Viongozi
    • Arumeru
      • Historia
      • Viongozi
    • Monduli
      • Historia
      • Viongozi
    • Karatu
      • Historia
      • Viongozi
    • Longido
      • Historia
      • Viongozi
    • Ngorongoro
      • Historia
      • Viongozi
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Arusha
    • Halmashauri ya Arusha
    • Halmashauri ya Meru
    • Halmashauri ya Monduli
    • Halmashauri ya Karatu
    • Halmashauri ya Longido
    • Halmashauri ya Ngorongoro
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo
    • Viwanda
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Ardhi
    • Utalii
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali
    • Habari
    • Matukio

WAZIRI ULEGA AUTAFUTIA SULUHU MGOGORO WA WAFUGAJI NA KIWANDA CHA ELIA FOOD. LONGIDO

Posted on: November 17th, 2023

Na Mwandishi wetu


Kufuatia malalamiko ya muda mrefu ya Kiwanda cha Elia Food kilichopo Wilayani Longido, mkoani Arusha kutokupata malighafi kwa ajili ya kuchakata nyama, Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Abdallah Ulega amefika Wilayani humo na kukutana na wafanyabiashara wa mifugo pamoja na Uongozi wa Kiwanda hicho kutafuta suluhu ya changamoto hiyo.


Akiongea katika mkutano ambao ulihusisha uongozi wa Mkoa, muwekezaji wa kiwanda hicho na wafanyabiashara wa mifugo uliofanyika wilayani humo Novemba 16, 2023, Waziri Ulega aliwaeleza kuwa lengo la kukutana nao ni kutaka kujua kwanini wafanyabiashara hao wa mifugo hawaendi kuuza mifugo yao katika kiwanda hicho na badala yake wanakwenda kuiuza nchi jirani.


Baada ya kusikiliza maoni mbalimbali kutoka kwa wafanyabiashara ya kwanini hawaendi kuuza mifugo yao katika kiwanda hicho, Waziri Ulega aliamua kuchukua hatua kadhaa za kusuluhisha mgogoro huo.


Hatua ya kwanza aliyoichukua ameelekeza iundwe timu ya Wataalam itakayokuwa chini ya Katibu Tawala wa Mkoa wa Arusha kwa kushirikiana na Wataalamu kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Meneja wa Mamlaka ya Mapato (TRA) wa Mkoa na wananchi wazoefu wa biashara ya mifugo ili kutafuta majawabu ya kutatua changamoto hizo ndani ya wiki mbili na kuwasilisha taarifa kwake.


Aidha, katika kikao hicho alimuagiza Afisa kutoka Benki ya Maendeleo ya Kilimo (TADB) kuhakikisha wanafungua tawi la benki hiyo Mkoani Arusha ili iwe rahisi kwa wafanyabiashara ya mifugo kupata mitaji kwa urahisi.


Halikadhalika, Waziri Ulega aliutaka uongozi wa Kiwanda hicho kuachana na tabia ya kuwakopa wafanyabiashara ya mifugo kwani kwa kufanya hivyo kunapelekea wafanyabiashara hao kutafuta sehemu ambapo wanauza mifugo yao bila kukopwa.


Awali, wakati wakitoa maoni yao, Wafanyabiashara hao walisema kuwa changamoto kubwa inayowafanya wasipeleke mifugo yao katika kiwanda hicho ni kubadilika badilika kwa bei, biashara kufanyika kwa mkopo na kukosekana kwa uwazi wakati wa kupima uzito wa mifugo.


Kwa upande wake, Mmiliki wa Kiwanda cha Elia Food, Bw. Shabbir Virjee aliishukuru Serikali ya Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuwapa kibali cha kuuza ngozi nje ya nchi na kusema kuwa biashara hiyo inaenda vizuri.


Aidha, alibainisha kuwa pamoja na biashara hiyo ya ngozi kwenda vizuri hata hivyo kuna changamoto ya ubora kutokana na baadhi ya ngozi hizo kuchorwa alama kubwa na wafugaji.



Tangazo

  • TAZAMA MATOKEO YA MTIHANI WA MOCK MKOA DARASA LA SABA 1 July 06, 2023
  • MATOKEO YA MOCK MKOA DARASA LA SABA 2 July 07, 2023
  • TAZAMA MATOKEO YA MOCK MKOA KIDATO CHA NNE July 07, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONDA ASHUHUDIA UTIAJI SAINI UJENZI WA BARABARA YA ESO - LONGDON NA UKUMBI WA MIKUTANO ARUSHA.

    April 03, 2025
  • RC MAKONDA ATAKA KUPEWA MAJINA YA WATENDAJI WANAOCHOCHEA MIGOGORO YA KIJAMII.

    March 28, 2025
  • KAMPENI YA MSAADA WA KISHERIA NI MAONO NA MAELEKEZO YA RAIS SAMIA- WAZIRI NDUMBARO.

    March 28, 2025
  • OFISI YA MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI YAFANYIA KAZI MALALAMIKO WANANCHI WA MIANZINI ARUSHA.

    March 28, 2025
  • Angalia Zote

Video

UZINDUZI WA BARABARA YA WASO-SALE
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • SALARY SLIP
  • Taarifa ya Mapato
  • Taarifa za Shule (SIS)
  • Takwimu za Sekta ya Elimu (BEMIS)
  • Video

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Portal ya Watumishi
  • Takwimu
  • TANAPA

Watembeleaji

world map hits counter

Wasiliana Nasi

Mawaliliano mengine

   

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani
    • Maswali ya Mara kwa Mara

Hatimiliki ©2018 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Arusha. Haki Zote Zimehifadhiwa