• Complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
Arusha Regional

The United Republic of Tanzania President Office Regional Administration and Local Government Arusha Regional

  • Home
  • About Us
    • History
      • Chimbuko/Asili ya eneo
      • Orodha ya wakuu wa mikoa waliopita-Arusha
    • Dira na dhima
    • The basics
    • Strategies
  • Administration
    • Structure
    • Departments
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji Mali
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Maji
    • Units
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
  • District
    • Arusha
      • Historia
      • Viongozi
    • Arumeru
      • Historia
      • Viongozi
    • Monduli
      • Historia
      • Viongozi
    • Karatu
      • Historia
      • Viongozi
    • Longido
      • Historia
      • Viongozi
    • Ngorongoro
      • Historia
      • Viongozi
  • Councils
    • Arusha CC
    • Arusha DC
    • Meru DC
    • Monduli DC
    • Karatu DC
    • Longido DC
    • Ngorongoro DC
  • Investment Opportunities
    • Tourism
    • Livestock
    • Agricultre
    • Industrial
  • Our Service
    • Health
    • Education
    • Water
    • Land
    • Tourism
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Acts
    • Application Forms
  • Media Center
    • Press Release
    • Videos
    • Speeches
    • Photo Gallery
    • News
    • Events

WILAYA YA KARATU KUPATIWA MAGARI 2 YA KUBEBEA WAGONJWA

Posted on: May 16th, 2023

Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Mhe Dkt. Samia Suluhu Hassan imepanga kuikabidhi Magari mawili ya kubebea wagonjwa Wilaya ya Karatu.

Hayo yamesema na Makamu wa Rais Dkt. Philip Isdor Mpango wakati akiweka jiwe la msingi katika hospitali ya Wilaya ya Karatu.

"Serikali imeweka nguvu kubwa katika kuhakikisha miundombinu ya sekta ya afya inaimarika zaidi na kuwezesha utoaji wa huduma bora".

Aidha, Dkt.Mpango amesema ndani ya miezi miwili Serikali italeta watumishi wasiopungua 25 katika sekta afya ili kuzifanya hospitali hizo kuendelea kutoa huduma bora na kwa wakati.

Amewataka wananchi wa Karatu kuhakikisha wanaitunza hospitali hiyo iliyogharimu fedha nyingi na walinde vifaa vya hospitali hiyo.

Pia, Serikali inaendelea kuhakikisha hospitali za Wilaya zinatoa huduma bora ikiwemo upatikanaji wa Dawa na vifaa tiba na viongozi wa wilaya wavisimamie.

Amewataka wale wote watakaobainika wameiba vifaa wakamatwe na wafikishwe katika vyombo vya sheria kwani watakuwa wamehujumu uchumi wa nchi.

Kwa upande wake, Naibu Waziri wa Afya Dkt. Godwin Mollel amesema nguvu kubwa imewekwa na Serikali katika sekta ya afya na kiasi cha Trilioni 1.3 zilitolewa na Serikali kwa ajili ya kuboresha sekta ya afya katika miundombinu na vifaa tiba.

Naye Naibu Katibu Mkuu Tamisemi,anayeshughulikia suala la Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe, Dkt.Charles Mahera alitoa rai kwa wananchi kulinda vifaa vya hospitali kwani baadhi za  hospitali za wilaya vifaa huibiwa.

Awali Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Karatu, Rajabu Karia alisema hospitali hiyo imeanza kutoa huduma baada ya kukamilika kwa majengo tisa ikiwemo jengo la wagonjwa wa nje na jengo la maabara lakini pia wanatarajia kutoa huduma za uzazi ili wananchi waanze kujifungua katika hospitali hiyo

Alisema ingawa hospitali hiyo imeanza kutoa huduma lakini bado kunachangamo zinazoendelea ya upungufu wa watumishi pamoja na samani na vifaa tiba kweye majengo yaliyokamilika na kuongeza kuwa hospitali hiyo imegharimu sh.bilioni 3.379.

Uzinduzi wa hospitali ya wilaya ni miongoni mwa shughuli zilizofanywa katika ziara ya kikazi ya Makamu wa Rais Dkt. Mpango katika Wilaya ya Karatu.



Announcements

  • TAZAMA MATOKEO YA MTIHANI WA MOCK MKOA DARASA LA SABA 1 July 06, 2023
  • MATOKEO YA MOCK MKOA DARASA LA SABA 2 July 07, 2023
  • TAZAMA MATOKEO YA MOCK MKOA KIDATO CHA NNE July 07, 2023
  • View All

Latest News

  • RC MAKONDA ASHUHUDIA UTIAJI SAINI UJENZI WA BARABARA YA ESO - LONGDON NA UKUMBI WA MIKUTANO ARUSHA.

    April 03, 2025
  • RC MAKONDA ATAKA KUPEWA MAJINA YA WATENDAJI WANAOCHOCHEA MIGOGORO YA KIJAMII.

    March 28, 2025
  • KAMPENI YA MSAADA WA KISHERIA NI MAONO NA MAELEKEZO YA RAIS SAMIA- WAZIRI NDUMBARO.

    March 28, 2025
  • OFISI YA MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI YAFANYIA KAZI MALALAMIKO WANANCHI WA MIANZINI ARUSHA.

    March 28, 2025
  • View All

Video

UZINDUZI WA BARABARA YA WASO-SALE
More Videos

Quick Links

  • Guildlines Towards the use of ICT In Government
  • SALARY SLIP
  • Taarifa ya Mapato
  • Taarifa za Shule (SIS)
  • Takwimu za Sekta ya Elimu (BEMIS)
  • Video

Related Links

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Public Servant Portal
  • Takwimu
  • TANAPA

World visitors tracker

world map hits counter

Contact Us

Other Contacts

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Sitemap
    • FAQ

Copyright ©2017 Arusha Regional Comissioner's Office. All rights reserved.