• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Arusha Regional

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Mkoa
      • Chimbuko/Asili ya eneo
      • Orodha ya wakuu wa Mikoa
    • Dira na dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji Mali
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Wilaya
    • Arusha
      • Historia
      • Viongozi
    • Arumeru
      • Historia
      • Viongozi
    • Monduli
      • Historia
      • Viongozi
    • Karatu
      • Historia
      • Viongozi
    • Longido
      • Historia
      • Viongozi
    • Ngorongoro
      • Historia
      • Viongozi
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Arusha
    • Halmashauri ya Arusha
    • Halmashauri ya Meru
    • Halmashauri ya Monduli
    • Halmashauri ya Karatu
    • Halmashauri ya Longido
    • Halmashauri ya Ngorongoro
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo
    • Viwanda
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Ardhi
    • Utalii
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali
    • Habari
    • Matukio

DED MERU DC AHAMASISHA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA; KWENYE DIWANI CUP

Posted on: October 7th, 2024


Mkurugenzi Mtendaji na Msimamizi wa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa, Halmashauri ya Wilaya ya Meru, Mwl. Zainabu J. Makwinya, amewahamasisha wananchi wote wenye sifa kujitokeza kwa wingi  kujiandikisha kwenye Orodha ya Wapiga Kura ili kuwa na sifa wa kushiriki Uchaguzi wa Serikali za Mitaa Novemba 27,2024. 



 Mwl.Makwinya ametoa rai hiyo, akimwakilisha, Mkuu wa Wilaya ya Arumeru Mhe. Amir Mkalipa  kama Mgeni kwenye Ligi ya Mpira wa Miguu iliyoandaliwa na Diwani wa Kata ya Uwiro Mhe. Dauson Urio, Ligi  iliyopewa jina la DIWANI CUP.



Hata hivyo, Mwl. Makwinya amepata fursa kutoa elimu kwa wananchi wa Kata ya Uwiro kuhusu  uchaguzi wa Viongozi wa Serikali za Mitaa kwa ngazi ya vijiji na vitongoji pamoja na kueleza sifa za mpiga kura Kugombea kwenye Uchaguzi huo wa Serikali za Mitaa. 



"Katika halmashauri yetu, uchaguzi utahusisha Wenyeviti wa Vijiji na wenyeviti wa vitongoji na kila mwananchi anatakiw akutumia haki yake ya kikatiba ya kupiga kura kwa kujiandiskisha kwenye eneo analoishi kwenye vituo vilivyoanishwz kuanzia tarehe 11- 20 Oktoba 2024, kila mkazi mwenye umri wa kuanzia miaka 18 anapaswa kujiandikisha na hatimaye kupiga kura ifikapoNovemba 27,2024"Amesisitiza Mwl.Makwinya



Licha ya Mkurugenzi huyo kuwataka wananchi kuchagua viongozi wenye sifa wenye uwezo wa kusukuma gurudumu la maendeleo kwenye vijij8 na vitongoji vyao, amewahamsisha kugombea nafasi hizo ili kuaota kiongozi bora.



Naye, Afisa Uchaguzi halmashauri hiyo, Edward Bujune, amegawa vipeperushi  kwa wananchi vyenye maelezo yanayohusu uchaguzi wa Serikali za Mitaa, vikionyesha sifa za wagombea na wapiga kura pamoja na tarehe za kujiandikisha na tarehe ya Uchaguzi. 



Hata hivyo, Katika uhamasishaji huo uliofanyika katika Kata ya Uwiro wananchi wamepatiwa elimu ya utofauti wa kujiandikisha kwenye daftari la Wakazi na Vitambulisho vya Kura vitakavyotumika kwenye Uchaguzi Mkuu utakaofanyika mwakani 2025. 



Timu zilizoshiriki katika mashindano ya fainali ya DIWANI CUP ni Timu ya Kivumbi na Timu ya Kimulimuli ambapo  Timu ya Kimulimuli imeibuka Kidedea kwa mikwaju ya Penati goli 4-3  baada ya Mchuano mkali wa dakika 90 bila kufungana.



Mhe.Diwani Kata ya Uwiro Dauson Urio kwa niaba ya Wananchi wa Kata ya Uwiro yenye vijiji vitatu vya Kisimiri Juu, Kisimiri Chini na Uwiro ametoa shukrani kwa Mkurugenzi Mtendaji kwa kufika na kuhamasisha wananchi kushiriki kikamilifu katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa. 



"Serikali za Mitaa, Sauti ya Wananchi, Jitokeze kushiriki Uchaguzi".


Tangazo

  • TAZAMA MATOKEO YA MTIHANI WA MOCK MKOA DARASA LA SABA 1 July 06, 2023
  • MATOKEO YA MOCK MKOA DARASA LA SABA 2 July 07, 2023
  • TAZAMA MATOKEO YA MOCK MKOA KIDATO CHA NNE July 07, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONDA ASHUHUDIA UTIAJI SAINI UJENZI WA BARABARA YA ESO - LONGDON NA UKUMBI WA MIKUTANO ARUSHA.

    April 03, 2025
  • RC MAKONDA ATAKA KUPEWA MAJINA YA WATENDAJI WANAOCHOCHEA MIGOGORO YA KIJAMII.

    March 28, 2025
  • KAMPENI YA MSAADA WA KISHERIA NI MAONO NA MAELEKEZO YA RAIS SAMIA- WAZIRI NDUMBARO.

    March 28, 2025
  • OFISI YA MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI YAFANYIA KAZI MALALAMIKO WANANCHI WA MIANZINI ARUSHA.

    March 28, 2025
  • Angalia Zote

Video

UZINDUZI WA BARABARA YA WASO-SALE
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • SALARY SLIP
  • Taarifa ya Mapato
  • Taarifa za Shule (SIS)
  • Takwimu za Sekta ya Elimu (BEMIS)
  • Video

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Portal ya Watumishi
  • Takwimu
  • TANAPA

Watembeleaji

world map hits counter

Wasiliana Nasi

Mawaliliano mengine

   

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani
    • Maswali ya Mara kwa Mara

Hatimiliki ©2018 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Arusha. Haki Zote Zimehifadhiwa