• Complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
Arusha Regional

The United Republic of Tanzania President Office Regional Administration and Local Government Arusha Regional

  • Home
  • About Us
    • History
      • Chimbuko/Asili ya eneo
      • Orodha ya wakuu wa mikoa waliopita-Arusha
    • Dira na dhima
    • The basics
    • Strategies
  • Administration
    • Structure
    • Departments
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji Mali
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Maji
    • Units
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
  • District
    • Arusha
      • Historia
      • Viongozi
    • Arumeru
      • Historia
      • Viongozi
    • Monduli
      • Historia
      • Viongozi
    • Karatu
      • Historia
      • Viongozi
    • Longido
      • Historia
      • Viongozi
    • Ngorongoro
      • Historia
      • Viongozi
  • Councils
    • Arusha CC
    • Arusha DC
    • Meru DC
    • Monduli DC
    • Karatu DC
    • Longido DC
    • Ngorongoro DC
  • Investment Opportunities
    • Tourism
    • Livestock
    • Agricultre
    • Industrial
  • Our Service
    • Health
    • Education
    • Water
    • Land
    • Tourism
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Acts
    • Application Forms
  • Media Center
    • Press Release
    • Videos
    • Speeches
    • Photo Gallery
    • News
    • Events

ASILIMIA 95.38 YA VIJIJI VYOTE VYA MKOA WA ARUSHA VIMEFIKIWA NA UMEME WA REA..

Posted on: November 26th, 2023

Na Elinipa Lupembe.


Vijiji 351 vya mkoa wa Arusha, sawa na asilimia 95.38 vimefikiwa na miundombinu ya umeme, huku wakandarasi wakiendelea na kazi ya kukamilisha usambazaji wa umeme kwenye vijiji 17 vilivyosalia ili kukamilisha vijiji vyote 368 vya mkoa huo na kufikia asilimia 100.


Hayo yamethibitishwa na mkuu wa mkoa wa Arusha Mhe. John V.K Mongella, alipopata fursa ya kuzungumza, muda mfupi kabla ya kumkaribisha, Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Mhe. Dkt. Doto Mashaka Biteko, alipotembelea na kukagua maendeleo ya utekelezaji wa mradi wa Kituo cha Kupokea, Kupoza na Kusafirisha Umeme cha Lemuguru - mkoani Arusha.


Mhe. Mongella, kwa niaba ya wananchi wa mkoa huo,  ameishukuru Wizara ya Nishati na Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa kuijali Arusha, kwa kutoa  fedha nyingi za kutekeleza miradi ya maendeleo huku ikitoa kipaumbele kwa kutekeleza miradi mikubwa ya miundombinu ya umeme kupitia mradi wa umeme vijijini (REA), miradi ambayo  iko hatua za ukamilishaji na kuvifikia vijiji vyote 368 vya mkoa wa Arusha.


"Kwa sasa Mkoa wa Arusha unakamilisha ufungaji wa umeme kwenye vijiji 17 vilivyosalia, huku wakandarasi wakijikita katika kuendelea kusambaza umeme kwenye vitongoji na kuwafikia watumiaji, jambo ambalo linachochea ukuaji wa uchumi wa mtu mmoja mmoja na Taifa kwa ujumla wake" Ameweka wazi RC Mongella


Ameongeza kuwa matokeo ya uwepo wa umeme Arusha, yameanza kuonekana wazi, kupitia  mabadiliko katika pato la wananchi sio kwa kuwaka tuu, bali kukuza uchumi wa mkoa, huku uanziashwaji wa viwanda vidogo ukiendelea, na wananchi kulazimika kujikita katika shughuli za uzalishaji, shughuli zinazosababisha, uwepo wa amani na utulivu katika mkoa huo.


"Nikiri wazi kuwa, wananchi wa Arusha wamenufaika na utekelezaji wa miradi ya maendeleo, huku Ilani ya Chama cha Mapinduzi ya mwaka 2020 - 2025, ikitekelezwa kwa asilimia 100 na kufikia lengo la serikali la kuhakikisha huduma za Umeme,  zinawafikia wananchi kwenye maeneo yao hususani wananchi waishio vijijini" Amethibitisha Mhe. Mongella.


Awali mradi wa Kituo cha Umeme Lemuguru, unatekelzwa na serikali kwa gharama ya shilingi bilioni 14.295, ukiwa umefika asilimia 30 na unategemea kuhusambaza na  kuongeza upatikanaji wa huduma za umeme kwa  wananchi wa maeneo ya Longido, Monduli, Arumeru pamoja na Jiji la Arusha.

#ArushaFursaLukuki



Announcements

  • TAZAMA MATOKEO YA MTIHANI WA MOCK MKOA DARASA LA SABA 1 July 06, 2023
  • MATOKEO MTIHANI WA UTAMIRIFU (MOCK) 2025 DARASA LA SABA (VII)- MKOA WA ARUSHA June 07, 2025
  • MATOKEO YA MOCK MKOA DARASA LA SABA 2 July 07, 2023
  • TAZAMA MATOKEO YA MOCK MKOA KIDATO CHA NNE July 07, 2023
  • View All

Latest News

  • KARIBU ARUSHA Mhe. KENAN LABAN KIHONGOSI MKUU WA MKOA WA ARUSHA

    June 26, 2025
  • KARIBU ARUSHA Mhe. KENAN LABAN KIHONGOSI MKUU WA MKOA WA ARUSHA

    June 26, 2025
  • SIKU YA KWANZA; WAKAZI WA ARUSHA WAJITOKEZA KWENYE KAMBI YA MADAKTARI BINGWA NA MABINGWA WABOBEZI

    June 23, 2025
  • RC MAKONDA ASHIRIKI MARATHON YA KKKT 2025

    June 21, 2025
  • View All

Video

UZINDUZI WA BARABARA YA WASO-SALE
More Videos

Quick Links

  • Guildlines Towards the use of ICT In Government
  • SALARY SLIP
  • Taarifa ya Mapato
  • Taarifa za Shule (SIS)
  • Takwimu za Sekta ya Elimu (BEMIS)
  • Video

Related Links

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Public Servant Portal
  • Takwimu
  • TANAPA

World visitors tracker

world map hits counter

Contact Us

Other Contacts

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Sitemap
    • FAQ

Copyright ©2017 Arusha Regional Comissioner's Office. All rights reserved.