• Complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
Arusha Regional

The United Republic of Tanzania President Office Regional Administration and Local Government Arusha Regional

  • Home
  • About Us
    • History
      • Chimbuko/Asili ya eneo
      • Orodha ya wakuu wa mikoa waliopita-Arusha
    • Dira na dhima
    • The basics
    • Strategies
  • Administration
    • Structure
    • Departments
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji Mali
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Maji
    • Units
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
  • District
    • Arusha
      • Historia
      • Viongozi
    • Arumeru
      • Historia
      • Viongozi
    • Monduli
      • Historia
      • Viongozi
    • Karatu
      • Historia
      • Viongozi
    • Longido
      • Historia
      • Viongozi
    • Ngorongoro
      • Historia
      • Viongozi
  • Councils
    • Arusha CC
    • Arusha DC
    • Meru DC
    • Monduli DC
    • Karatu DC
    • Longido DC
    • Ngorongoro DC
  • Investment Opportunities
    • Tourism
    • Livestock
    • Agricultre
    • Industrial
  • Our Service
    • Health
    • Education
    • Water
    • Land
    • Tourism
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Acts
    • Application Forms
  • Media Center
    • Press Release
    • Videos
    • Speeches
    • Photo Gallery
    • News
    • Events

DIWANI WA KATA YA KIUTU NI MFANO WA KUIGWA; ATOA ENEO LA UJENZI WA SHULE

Posted on: October 3rd, 2024


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais-TAMISEMI Mhe. Mohamed Mchengerwa amewataka Waheshimiwa Madiwani nchini kuiga mfano wa Diwani wa Kata ya Kiutu Mhe. Malaki Malambo aliyetoa kiwanja chenye ukubwa wa zaidi ya mita za mraba 6,400 kwa ajili ya kujenga shule ya Sekondari Kiutu Halmashauri ya Wilaya ya Arusha.



Mhe. Mchengerwa ametoa wito huo kwa madiwani wote nchini, akiwa kwenye ziara yake ya kikazi yenye lengo la kukagua na kuhimiza utekelezaji wa miradi ya maendeleo katika Halmashauri za Mkoa wa Arusha.



Amesisistiza kuwa, kitendo cha Diwani wa Kata ya Kiutu Mhe. Malambo kutoa kiwanja chake ni ishara ya upendo wa dhati alionao kwa wananchi ambao walimchagua ili awaongoze na kuwaletea maendeleo.



“Ninawaomba Madiwani nchini wengine kuiga mfano mzuri wa Mhe. Malambo aliyejitoa kwa wananchi wake kwa kutoa kiwanja kilichowezesha ujenzi wa shule ya Sekondari Kiutu, hii ndio uhalisia wa kuwatu’ikia wananchi". Amesisitiza.



Ili kuunga mkono jitihada wa Mhe. Malambo na wakazi wa mkoa wa Arusha, Waziri Mchengerwa ameanisha kuwa Ofisi ya Rais-TAMISEMI itafanya mchakato wa kuwezesha kukamilisha ujenzi wa jengo la Shule ya Kiutu ili shule hiyo mwakani ipokea wanafunzi zaidi ya 500 tofauti na mwaka huu ambapo imepokea wanafunzi 400. 



Mhe. Mchengerwa amesema majengo 8 yaliyokamilika hayawezi kuchukua wanafunzi zaidi ya 400, hivyo kuna uhitaji mkubwa wa kukamilisha majengo yaliyosalia ili wanafunzi wapate miundombinu bora na rafiki ya kuwawezesha kutimiza ndoto zao.



“Nikihitimisha ziara yangu, Mkurugenzi wa Idara ya Elimu Ofisi ya Rais-TAMISEMI aje na timu yake kufanya tathmini ya gharama zinazohitajika ili tuwasilishe ombi la fedha kwa Mhe. Rais na hatimaye tuweze kukamilisha ujenzi wa shule hiyo,” Mhe. Mchengerwa amehimiza.



Waziri Mchengerwa yupo mkoani Arusha kwa ajili ya ziara ya kikazi iliyolenga kukagua miradi ya maendeleo na kuhimiza uwajibikaji kwa wasimasmizi wa miradi hiyo ili iweze kukamilika kwa wakati.


Announcements

  • TAZAMA MATOKEO YA MTIHANI WA MOCK MKOA DARASA LA SABA 1 July 06, 2023
  • MATOKEO YA MOCK MKOA DARASA LA SABA 2 July 07, 2023
  • TAZAMA MATOKEO YA MOCK MKOA KIDATO CHA NNE July 07, 2023
  • View All

Latest News

  • RC MAKONDA AFUNGUA MKUTANO WA 33 WA WAKUU WA MAJESHI YA ULINZI (SADC).

    May 30, 2025
  • SAMIA MOTOCROSS CHAMPIONSHIP KUREJEA MSIMU WA PILI JULAI 12, 2025

    May 27, 2025
  • MKOA WA ARUSHA KUWA MWENYEJI WA MKUTANO MKUBWA WA WAKUU WA MAJESHI WA SADC

    May 25, 2025
  • UJENZI WA UWANJA WA AFCON ARUSHA SIO MICHEZO TU, NI FURSA YA KIUCHUMI

    May 24, 2025
  • View All

Video

UZINDUZI WA BARABARA YA WASO-SALE
More Videos

Quick Links

  • Guildlines Towards the use of ICT In Government
  • SALARY SLIP
  • Taarifa ya Mapato
  • Taarifa za Shule (SIS)
  • Takwimu za Sekta ya Elimu (BEMIS)
  • Video

Related Links

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Public Servant Portal
  • Takwimu
  • TANAPA

World visitors tracker

world map hits counter

Contact Us

Other Contacts

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Sitemap
    • FAQ

Copyright ©2017 Arusha Regional Comissioner's Office. All rights reserved.