• Complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
Arusha Regional

The United Republic of Tanzania President Office Regional Administration and Local Government Arusha Regional

  • Home
  • About Us
    • History
      • Chimbuko/Asili ya eneo
      • Orodha ya wakuu wa mikoa waliopita-Arusha
    • Dira na dhima
    • The basics
    • Strategies
  • Administration
    • Structure
    • Departments
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji Mali
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Maji
    • Units
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
  • District
    • Arusha
      • Historia
      • Viongozi
    • Arumeru
      • Historia
      • Viongozi
    • Monduli
      • Historia
      • Viongozi
    • Karatu
      • Historia
      • Viongozi
    • Longido
      • Historia
      • Viongozi
    • Ngorongoro
      • Historia
      • Viongozi
  • Councils
    • Arusha CC
    • Arusha DC
    • Meru DC
    • Monduli DC
    • Karatu DC
    • Longido DC
    • Ngorongoro DC
  • Investment Opportunities
    • Tourism
    • Livestock
    • Agricultre
    • Industrial
  • Our Service
    • Health
    • Education
    • Water
    • Land
    • Tourism
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Acts
    • Application Forms
  • Media Center
    • Press Release
    • Videos
    • Speeches
    • Photo Gallery
    • News
    • Events

Rais Magufuli Azindua Kituo cha Polisi cha Utalii

Posted on: April 7th, 2018

Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania mheshimiwa Dokta John Pombe Joseph Magufuli, ametoa Bilioni 10 kwa ajiri ya ujenzi wa nyumba za polisi wa vyeo vya chini nchi nzima.

Ameyasema hayo alipokuwa akizungumza na jeshi la polisi la mkoa wa Arusha katika sherehe za kuzindua  ofisi ya kidiplomasia ya utalii,Nyumba za makazi ya polisi na vituo 2 vya polisi wilayani Arusha.

Amesema kutokana na juhudi zilizofanywa na mkoa wa Arusha wa kujenga nyumba za polisi 31 baada ya nyumba 13 kuungua na moto mnamo Septemba 2017 na kusababisha familia 14 kukosa makazi.

Amewataka wakuu wa Mikoa wengine nchini kuiga mfano huo wa kujenga nyumba za polisi kwa  kuwashirikisha wadau mbalimbali kwani zilizoungua ni 13 na zimejengwa 31 zaidi ya zilizoungua.

Hata hivyo amewashauri pia wabunge watumie kiasi cha fedha cha mfuko wa jimbo katika kusaidia kujenga nyumba za polisi katika majimbo yao badala ya kuwaachia wakuu wa mikoa peke yao.

Aidha, Magufuli ametoa ajira 1500 ya wahitimu wa jeshi la kujenga Taifa(JKT) kuajiriwa katika jeshi la polisi, ili kuongeza nguvu zaidi katika maeneo mbalimbali ya nchi katika kulinda usalama.

Amelitaka jeshi la polisi kuendelea kuchapa kazi kwa bidii kwani amefurahishwa na maonyesha yaliyoonyeshwa katika sherehe hizo ambayo yametoa picha nzuri kwa nchi kuwa jeshi la polisi lipo imara na yeye ataendelea kuwaunga mkono kwa kila watachoamua kufanya.

Magufuri amelitaka jeshi la polisi nchini kurekebisha mapungufu madogo madogo yaliyojitokeza katika jesho hilo yakiwepo ya rushwa na uonevu kwa wananchi ambayo yamekuwa yakichafua jina la jesho hilo kwani yanafanywa na baadhi ya polisi.

Akisoma taarifa fupi ya ujenzi Mkuu wa jeshi la polisi nchini IGP Simon Sirro amesema ujenzi wa kituo cha polisi cha kidiplomasi kimegharimu kiasi cha shilingi milioni 193 ambapo ni michango kutoka kwa wadau na serikali.

Aidha, katika ujenzi wa kituo cha polisi cha Murieti kimegharimu kiasi cha milioni 260 na ujenzi wa nyumba za polisi 31 zimegharimu kiasi cha milioni 550 ambapo milioni 250 zimetoka serikalini,milioni 50 zimetolewa na polisi na wadau mbalimbali wamechangia kiasi cha milioni 250.

Amesema jeshi la polisi nchini limeendelea kulinda usalama wa raia na mali zao na hivyo kupelekea kupunguza matukio ya uharifu kwa kiasi kikubwa na hata pia kudhibiti ajari za barabara kwa kiwango kikubwa.

Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mrisho Gambo amemshukuru Rais kwa juhudi zake alizozifanya katika kuleta maendeleo kwa mkoa wa Arusha katika nyanja mbalimbali hasa upatikanaji wa maji safi, ujenzi wa barabara,uboreshaji wa huduma za afya na kuboresha elimu kwa ujumla.

Aidha, amesema mkoa wa Arusha umeendelea kuleta maboresho zaidi katika sekta ya elimu kwa kuandaa utaratibu wa kutunga mtihani mmoja kwa shule zote za mkoa wa Arusha,ambapo awali kila shule ilikuwa inaanda mitihani yake.

Rais Magufuli yupo mkoani Arusha kwa ziara ya kikazi ya siku 2 ambapo alitokea mkoani Manyara huko  alikabidhiwa ukuta wa machimbo ya Mirerani na sasa anaendelea na ziara  yake mkoani Arusha.

Announcements

  • TAZAMA MATOKEO YA MTIHANI WA MOCK MKOA DARASA LA SABA 1 July 06, 2023
  • MATOKEO YA MOCK MKOA DARASA LA SABA 2 July 07, 2023
  • TAZAMA MATOKEO YA MOCK MKOA KIDATO CHA NNE July 07, 2023
  • View All

Latest News

  • RC MAKONDA ASHUHUDIA UTIAJI SAINI UJENZI WA BARABARA YA ESO - LONGDON NA UKUMBI WA MIKUTANO ARUSHA.

    April 03, 2025
  • RC MAKONDA ATAKA KUPEWA MAJINA YA WATENDAJI WANAOCHOCHEA MIGOGORO YA KIJAMII.

    March 28, 2025
  • KAMPENI YA MSAADA WA KISHERIA NI MAONO NA MAELEKEZO YA RAIS SAMIA- WAZIRI NDUMBARO.

    March 28, 2025
  • OFISI YA MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI YAFANYIA KAZI MALALAMIKO WANANCHI WA MIANZINI ARUSHA.

    March 28, 2025
  • View All

Video

UZINDUZI WA BARABARA YA WASO-SALE
More Videos

Quick Links

  • Guildlines Towards the use of ICT In Government
  • SALARY SLIP
  • Taarifa ya Mapato
  • Taarifa za Shule (SIS)
  • Takwimu za Sekta ya Elimu (BEMIS)
  • Video

Related Links

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Public Servant Portal
  • Takwimu
  • TANAPA

World visitors tracker

world map hits counter

Contact Us

Other Contacts

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Sitemap
    • FAQ

Copyright ©2017 Arusha Regional Comissioner's Office. All rights reserved.