• Complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
Arusha Regional

The United Republic of Tanzania President Office Regional Administration and Local Government Arusha Regional

  • Home
  • About Us
    • History
      • Chimbuko/Asili ya eneo
      • Orodha ya wakuu wa mikoa waliopita-Arusha
    • Dira na dhima
    • The basics
    • Strategies
  • Administration
    • Structure
    • Departments
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji Mali
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Maji
    • Units
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
  • District
    • Arusha
      • Historia
      • Viongozi
    • Arumeru
      • Historia
      • Viongozi
    • Monduli
      • Historia
      • Viongozi
    • Karatu
      • Historia
      • Viongozi
    • Longido
      • Historia
      • Viongozi
    • Ngorongoro
      • Historia
      • Viongozi
  • Councils
    • Arusha CC
    • Arusha DC
    • Meru DC
    • Monduli DC
    • Karatu DC
    • Longido DC
    • Ngorongoro DC
  • Investment Opportunities
    • Tourism
    • Livestock
    • Agricultre
    • Industrial
  • Our Service
    • Health
    • Education
    • Water
    • Land
    • Tourism
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Acts
    • Application Forms
  • Media Center
    • Press Release
    • Videos
    • Speeches
    • Photo Gallery
    • News
    • Events

WATENDAJI WA KATA WAMETAKIWA KUZIFAHAMU BAJETI NA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZOTE  ZA MAENDELEO KWENYE KATA ZAO

Posted on: June 4th, 2024

Na Elinipa Lupembe

Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. Paul Christian Makonda, amewaagiza Maofisa Watendaji wa Kata zote za Mkoa wa Arusha kufahamu bajeti ya mapato na matumizi ya Kata husika kwa mwaka mzima.

Mhe. Makonda ametoa agizo hilo wakati akisikiliza kero na changamoto za wananchi wa Kata ya Mateves, kufuatia agizo la Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi Tanzania, Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi la kumtaka kurudi kata ya Mateves ili kusikiliza kero na malalamiko ya wananchi hao, ambapo Mhe. Makonda amerudi leo mapema  Juni 04, 2024.

Mhe. Makonda amewaagiza Maofisa hao kuhakikisha wanazifahamu vema bajeti na mipango ya kata zao kwa mwaka husika pamoja na utekelezaji wa shughuli na miradi ya maendeleo iliyotekelezwa na inayoendelea kutekelezwa kwenye kata husika huku wakifahamu muda wa utekelezaji wa miradi hiyo.

Amefafanua kuwa, kila Mtendaji anatakiwa kufahamu aina ya miradi iliyotekelezwa kwenye kata husika na gharama zake kisekta huku mikataba ya miradi hiyo, kiasi cha fedha alicholipwa mkandarasi na wazabuni waliotekeleza miradi, idadi ya wanufaika wa miradi hiyo pamoja na tija ya miradi kwa wanufaika.

"Ninakerwa na uwajibikaji na ufanisi mdogo wa baadhi wa watendaji wa Serikali za mitaa na vijiji, baadhi yao wamekosa sifa za kuwatumikia wananchi kutokana na uwajibikaji mdogo kwenye vituo vyao vya kazi, unaosababisha kero na malalamiko mengi kwa wananchi na kuichukia Serikali" Amebainisha Mhe.Makonda.


Hata hivyo Mhe. Makonda ameahidi kuanza kufanya ziara ya kata kwa kata mkoani Arusha na kuwataka Maofisa hao wa kata kujiandaa kutoa taarifa za utekelezaji wa shughuli wa maendeleo za kata zao wakati wa ziara hiyo maalum ya kusikiliza kero na malalamiko ya wananchi. 

#ArushaNaUtalii

#kaziinaendelea

Announcements

  • TAZAMA MATOKEO YA MTIHANI WA MOCK MKOA DARASA LA SABA 1 July 06, 2023
  • MATOKEO YA MOCK MKOA DARASA LA SABA 2 July 07, 2023
  • TAZAMA MATOKEO YA MOCK MKOA KIDATO CHA NNE July 07, 2023
  • View All

Latest News

  • RC MAKONDA AFUNGUA MKUTANO WA 33 WA WAKUU WA MAJESHI YA ULINZI (SADC).

    May 30, 2025
  • SAMIA MOTOCROSS CHAMPIONSHIP KUREJEA MSIMU WA PILI JULAI 12, 2025

    May 27, 2025
  • MKOA WA ARUSHA KUWA MWENYEJI WA MKUTANO MKUBWA WA WAKUU WA MAJESHI WA SADC

    May 25, 2025
  • UJENZI WA UWANJA WA AFCON ARUSHA SIO MICHEZO TU, NI FURSA YA KIUCHUMI

    May 24, 2025
  • View All

Video

UZINDUZI WA BARABARA YA WASO-SALE
More Videos

Quick Links

  • Guildlines Towards the use of ICT In Government
  • SALARY SLIP
  • Taarifa ya Mapato
  • Taarifa za Shule (SIS)
  • Takwimu za Sekta ya Elimu (BEMIS)
  • Video

Related Links

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Public Servant Portal
  • Takwimu
  • TANAPA

World visitors tracker

world map hits counter

Contact Us

Other Contacts

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Sitemap
    • FAQ

Copyright ©2017 Arusha Regional Comissioner's Office. All rights reserved.