• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Arusha Regional

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Mkoa
      • Chimbuko/Asili ya eneo
      • Orodha ya wakuu wa Mikoa
    • Dira na dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji Mali
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Wilaya
    • Arusha
      • Historia
      • Viongozi
    • Arumeru
      • Historia
      • Viongozi
    • Monduli
      • Historia
      • Viongozi
    • Karatu
      • Historia
      • Viongozi
    • Longido
      • Historia
      • Viongozi
    • Ngorongoro
      • Historia
      • Viongozi
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Arusha
    • Halmashauri ya Arusha
    • Halmashauri ya Meru
    • Halmashauri ya Monduli
    • Halmashauri ya Karatu
    • Halmashauri ya Longido
    • Halmashauri ya Ngorongoro
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo
    • Viwanda
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Ardhi
    • Utalii
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali
    • Habari
    • Matukio

Afya

 Utangulizi

Kuhusu Vituo vya Kutolea huduma ya Afya, Serikali ya Mkoa iliendelea kuweka msisitizo katika upatikanaji wa huduma bora za afya kupitia jumla ya vituo 408 vinavyotoa huduma za Afya, zikiwemo hospitali 19, vituo vya afya 61 na zahanati 328.  Mkoa umeweka jitihada za dhati katika kuongeza idadi kwa idadi ya vituo vya kutolea huduma za Afya kutoka vituo 392 mwaka 2020 hadi vituo 408 mwaka 2021 hadi Machi, 2022. Kati ya vituo 408 vya kutolea huduma vilivyopo, Serikali inamiliki vituo 234 (57%), taasisi za umma 15 (4%), watu na taasisi binafsi vituo 159 (39%).

Miradi ya Afya kupitia Mapato ya Ndani.

Katika kuhakikisha kuwa huduma za Afya kwa wananchi zinaboreshwa, Serikali ilibuni na kutekeleza mradi wa ujenzi na ukamilishaji miundombinu ya afya katika Halmashauri zote za Mkoa wa Arusha, kwa gharama ya Shilingi bilioni 3.8 zilitolewa kupitia fedha za Mapato ya Ndani ya Halmashauri na hadi kufikia mwezi Machi,2022 shilingi bilioni 1.32 zimetumika sawa na asilimia 34.8. Vituo hivi viko katika hatua mbalimbali za ujenzi. Miradi iliyotekelezwa ni pamoja na ujenzi wa vituo vya afya vipya, Zananati, kuchangia ujenzi wa Hospitali za Wilaya na ujenzi wa miundombinu mbalimbali ya afya katika vituo vya kutolea huduma za afya.

Miradi ya Afya kupitia Fedha za Ruzuku ya Serikali Kuu.

Mkoa wa Arusha kwa kipindi cha Julai hadi Feb, 2022 umepokea fedha za ruzuku kwa ajili ya ujenzi wa miradi ya afya jumla ya shilingi bilioni 2.5.  Miradi ya afya inayohusika ni pomoja na ukamilishaji wa vituo vya Afya, ukamilishaji wa nyumba za watumishi wa afya, ujenzi na ukarabati wa Zahanati pamoja na ujenzi wa Hospitali za Wilaya ikijumuisha Hospitali ya Jiji la Arusha.

 Miradi ya Afya kupitia Fedha za Tozo.

 Mkoa wa Arusha kwa kipindi cha Julai hadi Februari,2022 ulipokea fedha za TOZO jumla ya shilingi bilioni 1.75 ikiwa ni sawa na shilingi milioni 250 kwa  kila Halmashauri za Mkoa wa Arusha kwa ajili ya ujenzi wa vituo vya Afya kwa tarafa zisizokuwa na Vituo vya Afya. Hadi Machi,2022 jumla ya shilingi bilioni 1.34 zilikuwa zimetumika kwa ajili ya ujenzi na hatua zilizofikiwa ni kama zinavyooneshwa kwenye jedwali hapa chini.

Jedwali Na.9: Mchanganuo wa Vituo vya Afya vinavyojengwa kwa Fedha za TOZO

Halmashauri
Kata
Jina la
Mradi

Kiasi cha fedha kilichopokelewa

Kiasi cha fedha kilichotumika

Hatua ya utekelezaji

Arusha Jiji
Terrat
Kituo cha Afya Mkonoo

250,000,000.00

121,000,000.00

Upauzi
Arusha DC
Mwandeti
Kituo cha Afya Engalawon

250,000,000.00

152,060,678.00

Umaliziaji
Meru DC
King’ori
Kituo cha Afya Mareu

250,000,000.00

164,678,900.00

Umaliziaji
Longido DC
Ketumbeine
Kituo cha Afya Ketumbeine

250,000,000.00

237,000,000.00

Umaliziaji
Karatu DC
Baray
Kituo cha Afya Mbuga Nyekundu

250,000,000.00

219,000,000.00

Umaliziaji
Monduli DC
Kisongo
Kituo cha Afya NAFCO

250,000,000.00

240,453,438.00

Umaliziaji
Ngorongoro DC
Sale
Kituo cha Afya Sale

250,000,000.00

215,378,265.00

Umaliziaji

Jumla

1,750,000,000.00

1,349,571,281.00

 

Chanzo: Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Machi 2022

Miradi ya Afya kupitia fedha za UVIKO-19.

Mkoa wa Arusha kwa kipindi cha Julai hadi Machi,2022 ulipokea fedha za UVIKO-19 jumla ya shilingi bilioni 1.99  kwa ajili ya ujenzi wa Majengo ya Huduma za Dharura (EMD) kwa Halmashauri za Arusha Jiji, Meru, Ngorongoro na Karatu, ikiwa ni mgao wa shilingi milioni 300 kwa kila Halmashauri 3, Pamoja na Tshi Milioni 540 kwa kila  Halmashuri  shilingi milioni 90 kwa ajili ya ujenzi wa nyumba za watumishi idara ya afya kwa Halmashauri za Wilaya zote isipokuwa Jiji la Arusha. Miradi yote ilianzwa kutekelezwa mwezi Machi, 2022 ipo katika hatua mbalimbali ya utekelezaji.

 Aidha, Wilaya ya Longido imepokea kiasi cha shilingi milioni 250 kwa ajili ya Ujenzi wa vyumba vya Huduma za Wagonjwa Mahututi (ICU) ambao upo hatua ya awali ya ujenzi.

Uboreshaji wa huduma katika Hospitali ya Rufaa ya Mt Meru 

Juhudi za Serikali za kuboresha huduma za afya katika Hospitali i ya Rufaa ya Mkoa, Hospitali ya Rufaa ya Mount Meru imepokea jumla ya shillingi Bilioni 3.97 kwa ajili ya ununuzi wa vifaa tiba vya kisasa ambavyo havijawahi kuwepo katika hospitali hii tangu kuanzishwa kwake. Vifaa hivyo ni: -Vifaa vya Dharura shilingi milioni 771, Vifaa vya Huduma za wagonjwa Mahututi     Shilingi milioni 660, CT Scan   Shilingi Bilioni 2.3 na Digital X-ray Shilingi milioni 240.

Aidha, miradi yote hiyo inaendelea kutekelezwa katika hatua mbalimbali na itakapokamilika itaboresha huduma kwa wagonjwa wanaopata huduma katika Hospitali ya Rufaa na hivyo itapunguza rufaa ya baadhi ya magonjwa zinazopelekwa Hospitali za Muhimbili na KCMC.

Tangazo

  • TAZAMA MATOKEO YA MTIHANI WA MOCK MKOA DARASA LA SABA 1 July 06, 2023
  • MATOKEO YA MOCK MKOA DARASA LA SABA 2 July 07, 2023
  • TAZAMA MATOKEO YA MOCK MKOA KIDATO CHA NNE July 07, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONDA ASHUHUDIA UTIAJI SAINI UJENZI WA BARABARA YA ESO - LONGDON NA UKUMBI WA MIKUTANO ARUSHA.

    April 03, 2025
  • RC MAKONDA ATAKA KUPEWA MAJINA YA WATENDAJI WANAOCHOCHEA MIGOGORO YA KIJAMII.

    March 28, 2025
  • KAMPENI YA MSAADA WA KISHERIA NI MAONO NA MAELEKEZO YA RAIS SAMIA- WAZIRI NDUMBARO.

    March 28, 2025
  • OFISI YA MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI YAFANYIA KAZI MALALAMIKO WANANCHI WA MIANZINI ARUSHA.

    March 28, 2025
  • Angalia Zote

Video

UZINDUZI WA BARABARA YA WASO-SALE
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • SALARY SLIP
  • Taarifa ya Mapato
  • Taarifa za Shule (SIS)
  • Takwimu za Sekta ya Elimu (BEMIS)
  • Video

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Portal ya Watumishi
  • Takwimu
  • TANAPA

Watembeleaji

world map hits counter

Wasiliana Nasi

Mawaliliano mengine

   

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani
    • Maswali ya Mara kwa Mara

Hatimiliki ©2018 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Arusha. Haki Zote Zimehifadhiwa