• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Arusha Regional

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Mkoa
      • Chimbuko/Asili ya eneo
      • Orodha ya wakuu wa Mikoa
    • Dira na dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji Mali
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Wilaya
    • Arusha
      • Historia
      • Viongozi
    • Arumeru
      • Historia
      • Viongozi
    • Monduli
      • Historia
      • Viongozi
    • Karatu
      • Historia
      • Viongozi
    • Longido
      • Historia
      • Viongozi
    • Ngorongoro
      • Historia
      • Viongozi
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Arusha
    • Halmashauri ya Arusha
    • Halmashauri ya Meru
    • Halmashauri ya Monduli
    • Halmashauri ya Karatu
    • Halmashauri ya Longido
    • Halmashauri ya Ngorongoro
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo
    • Viwanda
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Ardhi
    • Utalii
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali
    • Habari
    • Matukio

Elimu

Utekelezaji wa Miradi ya Elimu kupitia Fedha za Mapato ya Ndani ya Halmashauri.

Mkoa wa Arusha umekuwa ukipokea fedha za utekelezaji wa Miradi ya Ujenzi na ukamilishaji wa miundo mbinu mbalimbali katika Shule za msingi na Sekondari, miradi hii imeboresha mazingira ya kujifunzia na kufundishia walimu. Miradi hii ni Ujenzi wa Madarasa, Mabweni, Matundu ya vyoo, Nyumba za Walimu, Maabara, Mabwalo, Ofisi za Walimu na Maktaba.

Katika kipindi cha mwezi Julai 2021- Februari 2022, Halmashauri za Mkoa wa Arusha zimetenga jumla ya shilingi milioni 884.15 kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu 158 katika Shule za Msingi. Hadi kufikia mwezi Machi, 2022, miundombinu 83 ilikuwa hatua ya ukamilishaji na miundombinu 75 ipo katika hatua mbalimbali za utekelezaji.

Kwa upande wa Elimu Sekondari, kwa kipindi cha mwezi Julai 2021 hadi Februari, 2022, Mkoa umetenga jumla ya shilingi bilioni 1.088 kwa ajili ya ujenzi wa jumla ya miundombinu 192 ya mabweni, vyumba vya madarasa, nyumba za watumishi, matundu ya vyoo, Maabara na majengo ya utawala katika Shule za Sekondari. Aidha, hadi kufikia Machi, 2022, jumla ya miundombinu 116 ipo hatua ya ukamilishaji na miundombinu 78 ipo katika hatua mbalimbali za utekelezaj

Utekelezaji wa Miradi ya Elimu kupitia Fedha za UVIKO-19

Ujenzi wa Madarasa ya Shule Shikizi

Mkoa wa Arusha ulipokea jumla ya shilingi bilioni 1.92 kwa ajili ya ujenzi wa madarasa 96 ya Shule Shikizi kutoka fedha za UVIKO-19. Hadi kufikia Machi, 2022 jumla ya madarasa 92 yalikuwa yamekamilika sawa na asilimia 95 ya madarasa yote shikizi. Aidha, fedha za madarasa 4 ya Shule Shikizi ya Wilaya ya Ngorongoro katika Tarafa ya Ngorongoro zimeshahamishiwa Wilaya ya Handeni.Ujenzi wa Madarasa ya Shule za Sekondari kupitia Fedha za UVIKO-19

Mkoa wa Arusha umepokea jumla ya shilingi bilioni 8.34 kwa ajili ya ujenzi wa madarasa 417 ya shule za sekondari. Hadi kufikia Machi, 2022, jumla ya madarasa 386 yalikuwa yamekamilika kwa asilimia 100 ikiwemo utengenezaji wa viti 50 na meza 50 kwa kila darasa. hii ni sawa na utekelezaji wa asilimia 93 ya madarasa yote. Madarasa 31 ya ghorofa kwa Halmashauri ya Jiji la Arusha (19) na Wilaya ya Arusha (12) yako katika hatua ya ukamilishaji kama kupaka rangi. Aidha, madarasa 12 ya Tarafa ya Ngorongoro katika Halmashauri ya Wilaya ya Ngorongoro yalikuwa hayajaanza ujenzi kutokana na kutopata kibali cha ujenzi kutoka Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro na fedha zake zimehamishiwa katika Halmashauri ya Handeni.

Ujenzi wa Mabweni ya Shule za Msingi  kupitia Fedha za UVIKO-19

Mkoa wa Arusha umepokea jumla ya shilingi milioni 160 kwa ajili ya ujenzi wa mabweni mawili kwa Shule za Msingi zenye Wanafunzi wenye Mahitaji Maalum kwa Wilaya za Ngorongoro na Meru. Bweni la Wilaya ya Meru lipo katika hatua ya upauzi na bweni la Wilaya ya Ngorongoro ambalo lipo kwenye Tarafa ya Ngorongoro halijaanza kujengwa kutokana na kukosa kibali kutoka Mamlaka ya Hifadhi ya Ngoron

Pamoja na mafanikio yalioyopatikana kutoka na fedha za UVIKO-19 zilizosaidia kujengwa vyumba vya madarasa, madarasa shikizi na mabweni katika shule maalumu, Sekta ya Elimu bado inaendela kunufaika na miradi mingine kupitia fedha za LANES, Ruzuku ya Serikali (TOZO), TEA na Mfuko wa Jimbo. Fedha hizo zote zimesaidia kuboresha miundombinu mbalimbali katika Shule za Msingi na Sekondari.  

Halmashauri za Arusha,

 Arusha Jiji na Monduli zilipokea jumla ya shilingi milioni 860.5 kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu 70. Hadi Machi 2022 jumla ya shilingi milioni 483.76 zilikuwa zimetumika kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu hiyo. Miundombinu hiyo ambayo ni madarasa, matundu ya vyoo na mifumo ya uvunaji maji ipo katika hatua mbalimbali za utekelezaji na kazi zinaendelea.

Ukamilishaji wa Vyumba vya Madarasa ya Sekondari kwa Fedha za TOZO

 Mkoa wa Arusha kutokana na fedha za Tozo ulipokea jumla ya shilingi milioni 162,500,000 kwa ajili ya ukamilishaji wa vyumba vya madarasa 13 ya Shule za Sekondari ambapo kila darasa lilipokea shilingi 12,500,000. Fedha hizi zilikuwa ni kwa ajili ya kumalizia vyumba vya madarasa vilivyojengwa kwa nguvu za wananchi miradi hiyo imekamilika.

Utekelezaji wa Miradi ya Elimu kupitia Fedha za Nje (EP4R).

Mkoa wa Arusha ulipokea kiasi cha shilingi milioni 508.62 fedha kutoka Vyanzo vya Nje (Foreign) kwa ajili ya utekelezaji wa jumla ya miundombinu 343 katika shule za Msingi na Sekondari ambapo kati ya miundombinu hiyo, vyumba vya madarasa ni 17, madawati 220, Hosteli 1, Nyumba ya Mwalimu 1 na matundu ya vyoo ni 102. Lengo ni kuboresha miundombinu na mazingira ya kujifunzia. Utekelezaji umefanyika katika Halmashauri za Arusha, Monduli na Ngorongoro na utekelezaji upo katika hatua za ukamilishaji.

 Utekelezaji wa Miradi ya Sekondari Kupitia Programu ya Kuboresha Elimu ya Sekondari (SEQUIP)

Mkoa wa Arusha umepokea jumla ya shilingi bilioni 4.7 kwa ajili ya ujenzi wa Shule za Sekondari mpya kumi (10) katika kata 10 zisizokuwa na Shule za Sekondari kupitia Program ya Kuboresha Elimu ya Sekondari (SEQUIP). Ujenzi wa shule hizi upo katika hatua mbalimbali za ukamilishaji.

Ujenzi wa Vyumba vya Maabara katika shule za Sekondari 

Kuhusu miundombinu ya shule za Sekondari, hususani ujenzi wa maabara za sayansi, Mkoa wa Arusha mwaka 2020 ulikuwa na vyumba vya maabara za 326 hata hivyo kufikia Machi, 2022 Mkoa umefanikiwa kujenga maabara 401 kwa mchanganuo zikiwemo ufuatao biolojia, 130 kemia 137, fizikia112 na Tehama 22.

Tangazo

  • TAZAMA MATOKEO YA MTIHANI WA MOCK MKOA DARASA LA SABA 1 July 06, 2023
  • MATOKEO YA MOCK MKOA DARASA LA SABA 2 July 07, 2023
  • TAZAMA MATOKEO YA MOCK MKOA KIDATO CHA NNE July 07, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONDA ASHUHUDIA UTIAJI SAINI UJENZI WA BARABARA YA ESO - LONGDON NA UKUMBI WA MIKUTANO ARUSHA.

    April 03, 2025
  • RC MAKONDA ATAKA KUPEWA MAJINA YA WATENDAJI WANAOCHOCHEA MIGOGORO YA KIJAMII.

    March 28, 2025
  • KAMPENI YA MSAADA WA KISHERIA NI MAONO NA MAELEKEZO YA RAIS SAMIA- WAZIRI NDUMBARO.

    March 28, 2025
  • OFISI YA MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI YAFANYIA KAZI MALALAMIKO WANANCHI WA MIANZINI ARUSHA.

    March 28, 2025
  • Angalia Zote

Video

UZINDUZI WA BARABARA YA WASO-SALE
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • SALARY SLIP
  • Taarifa ya Mapato
  • Taarifa za Shule (SIS)
  • Takwimu za Sekta ya Elimu (BEMIS)
  • Video

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Portal ya Watumishi
  • Takwimu
  • TANAPA

Watembeleaji

world map hits counter

Wasiliana Nasi

Mawaliliano mengine

   

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani
    • Maswali ya Mara kwa Mara

Hatimiliki ©2018 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Arusha. Haki Zote Zimehifadhiwa