• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Arusha Regional

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Mkoa
      • Chimbuko/Asili ya eneo
      • Orodha ya wakuu wa Mikoa
    • Dira na dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji Mali
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Wilaya
    • Arusha
      • Historia
      • Viongozi
    • Arumeru
      • Historia
      • Viongozi
    • Monduli
      • Historia
      • Viongozi
    • Karatu
      • Historia
      • Viongozi
    • Longido
      • Historia
      • Viongozi
    • Ngorongoro
      • Historia
      • Viongozi
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Arusha
    • Halmashauri ya Arusha
    • Halmashauri ya Meru
    • Halmashauri ya Monduli
    • Halmashauri ya Karatu
    • Halmashauri ya Longido
    • Halmashauri ya Ngorongoro
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo
    • Viwanda
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Ardhi
    • Utalii
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali
    • Habari
    • Matukio

RAIS SAMIA KUZIUNGANISHA MONDULI NA NGORONGORO KWA BARABARA YA LAMI..

Posted on: September 10th, 2025



 _Usanifu wakamilika, yatarajiwa kukuza utalii na uchumi wa Arusha_


Serikali ya awamu ya sita chini ya Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imeanza rasmi utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa barabara ya kiwango cha lami ya Mto wa Mbu- Engaruka, Engaruka- Ngaresero ili kukuza shughuli za kiuchumi na kijamii ikiwemo Utalii na Uwekezaji, barabara itakayoziunganisha Wilaya za Monduli na Ngorongoro.


Akizungumza na Viongozi wa dini, Mila na Serikali pamoja na Watendaji kuanzia ngazi ya Kitongoji Halmashauri ya Wilaya ya Monduli, leo Jumatano Septemba 10, 2025 wakati akihitimisha ziara yake Wilayani humo, Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. CPA Amos Gabriel Makalla amesema usanifu wa barabara hiyo ya Mto wa Mbu- Engaruka- Ngaresero yenye urefu wa Kilomita 74 umekamilika na hatua za kumpata Mkandarasi zimeshaanza.


"Lengo la Mhe. Rais na serikali yake ya awamu ya sita ni kutatua hili tatizo la muda mrefu na kuunganisha Wilaya za Monduli na Ngorongoro suala ambalo litavutia zaidi uwekezaji unaofanywa kwenye kiwanda cha Magadi soda Engaruka katika Wilaya ya Monduli pamoja na kutimiza dhamira njema ya kukuza utalii Mkoani Arusha kupitia Ziwa Natroni lililopo Wilaya ya Ngorongoro, Wana Monduli Mhe. Rais anatupenda sana." Amesema Mhe. CPA Makalla.


Aidha  CPA Makalla amefafanua kuwa barabara hiyo itajengwa kwa vipande vitatu ambavyo ni Kilomita 23 za Mto wa Mbu- Selela, Kilomita 27 za Selela- Engaruka pamoja na Kilomita 24 za Engaruka- Ngaresero, akiwataka Viongozi wa Wilaya hizo kusimamia kikamilifu mradi huo pamoja na miradi mingine inayotekelezwa kwenye maeneo yao ili iweze kukamilika kwa wakati na katika ubora uliokusudiwa.


Kadhalika CPA Makalla licha ya kuahidi kusimamia na kusukuma uharaka katika utekelezaji wa mradi huo, ameweka wazi kuwa Dkt. Samia ametoa shilingi Bilioni 17 kwaajili ya utekelezaji wa mradi wa skimu ya Umwagiliaji Wilayani Monduli, mradi ambao kukamilika kwake utanufaisha Vijiji zaidi ya kumi na moja, akisema Mkandarasi wa kutekeleza mradi huo tayari amepatikana na kazi itaanza hivi karibuni.


Tangazo

  • TAZAMA MATOKEO YA MTIHANI WA MOCK MKOA DARASA LA SABA 1 July 06, 2023
  • MATOKEO MTIHANI WA UTAMIRIFU (MOCK) 2025 DARASA LA SABA (VII)- MKOA WA ARUSHA June 07, 2025
  • MATOKEO YA MOCK MKOA DARASA LA SABA 2 July 07, 2023
  • TAZAMA MATOKEO YA MOCK MKOA KIDATO CHA NNE July 07, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKALLA AUNDA TUME KUFUATILIA SAKATA LA MACHINJIO NGORBOB ARUMERU..

    September 09, 2025
  • WAMAREKANI WATALII KWA WINGI TANZANIA- KAIMU BALOZI MAREKANI TANZANIA..

    September 11, 2025
  • RAIS SAMIA KUZIUNGANISHA MONDULI NA NGORONGORO KWA BARABARA YA LAMI..

    September 10, 2025
  • KILA LA KHERI DARASA LA SABA 2025..

    September 10, 2025
  • Angalia Zote

Video

UZINDUZI WA BARABARA YA WASO-SALE
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • SALARY SLIP
  • Taarifa ya Mapato
  • Taarifa za Shule (SIS)
  • Takwimu za Sekta ya Elimu (BEMIS)
  • Video

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Portal ya Watumishi
  • Takwimu
  • TANAPA

Watembeleaji

world map hits counter

Wasiliana Nasi

Mawaliliano mengine

   

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani
    • Maswali ya Mara kwa Mara

Hatimiliki ©2018 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Arusha. Haki Zote Zimehifadhiwa