• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Arusha Regional

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Mkoa
      • Chimbuko/Asili ya eneo
      • Orodha ya wakuu wa Mikoa
    • Dira na dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji Mali
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Wilaya
    • Arusha
      • Historia
      • Viongozi
    • Arumeru
      • Historia
      • Viongozi
    • Monduli
      • Historia
      • Viongozi
    • Karatu
      • Historia
      • Viongozi
    • Longido
      • Historia
      • Viongozi
    • Ngorongoro
      • Historia
      • Viongozi
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Arusha
    • Halmashauri ya Arusha
    • Halmashauri ya Meru
    • Halmashauri ya Monduli
    • Halmashauri ya Karatu
    • Halmashauri ya Longido
    • Halmashauri ya Ngorongoro
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo
    • Viwanda
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Ardhi
    • Utalii
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali
    • Habari
    • Matukio

KUWENI MARAFIKI WA WANANCHI

Posted on: November 23rd, 2021

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan  amelitaka jeshi la polisi kitengo cha usalama barabarani kujikita katika kufanya tafiti zitakazowesha kupata Suluhu za kudumu za kupunguza ajali za barabarani.

Maagizo hayo ameyatoa alipokuwa akifungua maadhimisho ya wiki ya nenda kwa usalama barabarani Kitaifa,Jijini Arusha.

Amesema zikifanyika tafiti nyingi za kitaalami zitasaidia kupata suluhu ya kudumu ya kupunguza ajali za barabarani au kuzuia kabisa ili kuokoa vijana wengi wanaopoteza maisha kwa wingi.

Ajali nyingi  za barabarani zaidi ya asilimia 90 zinasababishwa na makosa ya kibinadamu huku asilimia 3.2 za ajali zinatokana na ubovu wa magari na asilimia 1.3 ni ubovu wa Barabara.

Kutokana ma sababu hizo jumla ya watu waliopoteza maisha ndani ya miaka mitano ni 2220 kwa ajali za bodaboda, majerui 4402 na kwa mwaka vijana takribani 445 walikuwa wamepoteza maisha.

Pia, ajali zingine zilizotokana na basi zilikuwa 148 na daladala 142, kutokana na takwimu hizo bado bodaboda wanaongoza kwa vifo nchini, hivyo elimu iendelee kutolewa zaidi kwao.

Vile vile amesisitiza katika ukaguzi wa magari kwa njia za kisasa hasa katika zoezi la utoaji stika za  nenda kwa usalama katika magari ili kurahisha ukaguzi kwa magari mengi na kulipatia fedha jeshi la polisi zitakazo saidia kuendesha  shughuli zao mbalimbali.

Nae, Katibu mtendaji wa balaza la Taifa la usalama barabarani  kamishina msaidizi mwandamizi wa polisi SACP Wilbrod Mutafungwa amesema, hadi sasa ajali za barabarani zinapungua kwa kiasi kikubwa ukilinganisha na miaka ya nyuma.

Kwa mwaka 2020  jumla ya ajali za barabarani 1383 zilitokea na 2021ajali zilikuwa1187 ambazo ni punguzo la ajali 201 sawa na asilimia 14.5, huku vifo vikiwa 949 mwaka 2020 na 2021 vilikuwa 900 sawa na  punguzo la vifo  49 sawa na asilimia 5.2.

Pia, katika mwaka huo majerui walikuwa 1672  kwa mwaka 2020 na 2021 walikuwa 1405 kwa  punguzo la  majerui 267 sawa na asilimia 16.

Ameainisha sababu kubwa za ajali za barabarani ni ubovu wa Barabara, kutovaa kofia ngumu kwa madereva, kutofuata Sheria za barabarani na nyingine nyingi.

Aidha, amewaomba wadau wa usalama barabarani kuendelea kuunga mkono juhudi za kuzuia ajali za barabarani.

Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. John Mongella amemshukuru Rais Samia Suluhu kwa kutoa fedha takribani Bilioni 20.6 kwa Wakala wa  barabara Tanzania (TANROADS) Arusha na bilioni 19 kwa Wakala wa barabara Vijijini na mjini (TARURA) kwa Mkoa wa Arusha ili kuboresha Barabara na kulinda usalama wa watu.

Maadhimisho ya wiki ya nenda kwa usalama barabarani yamezinduliwa rasmi leo Novemba 23,2021 na  yanatarajiwa kufungwa Novemba 28, 2021 ambapo mara ya mwisho yaliadhimishwa 2017 Mkoani Kilimanjaro na kauli mbiu ya mwaka huu ni" Jali usalama wako na wengine barabarani".



Tangazo

  • TAZAMA MATOKEO YA MTIHANI WA MOCK MKOA DARASA LA SABA 1 July 06, 2023
  • MATOKEO YA MOCK MKOA DARASA LA SABA 2 July 07, 2023
  • TAZAMA MATOKEO YA MOCK MKOA KIDATO CHA NNE July 07, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONDA ASHUHUDIA UTIAJI SAINI UJENZI WA BARABARA YA ESO - LONGDON NA UKUMBI WA MIKUTANO ARUSHA.

    April 03, 2025
  • RC MAKONDA ATAKA KUPEWA MAJINA YA WATENDAJI WANAOCHOCHEA MIGOGORO YA KIJAMII.

    March 28, 2025
  • KAMPENI YA MSAADA WA KISHERIA NI MAONO NA MAELEKEZO YA RAIS SAMIA- WAZIRI NDUMBARO.

    March 28, 2025
  • OFISI YA MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI YAFANYIA KAZI MALALAMIKO WANANCHI WA MIANZINI ARUSHA.

    March 28, 2025
  • Angalia Zote

Video

UZINDUZI WA BARABARA YA WASO-SALE
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • SALARY SLIP
  • Taarifa ya Mapato
  • Taarifa za Shule (SIS)
  • Takwimu za Sekta ya Elimu (BEMIS)
  • Video

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Portal ya Watumishi
  • Takwimu
  • TANAPA

Watembeleaji

world map hits counter

Wasiliana Nasi

Mawaliliano mengine

   

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani
    • Maswali ya Mara kwa Mara

Hatimiliki ©2018 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Arusha. Haki Zote Zimehifadhiwa