• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Arusha Regional

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Mkoa
      • Chimbuko/Asili ya eneo
      • Orodha ya wakuu wa Mikoa
    • Dira na dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji Mali
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Wilaya
    • Arusha
      • Historia
      • Viongozi
    • Arumeru
      • Historia
      • Viongozi
    • Monduli
      • Historia
      • Viongozi
    • Karatu
      • Historia
      • Viongozi
    • Longido
      • Historia
      • Viongozi
    • Ngorongoro
      • Historia
      • Viongozi
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Arusha
    • Halmashauri ya Arusha
    • Halmashauri ya Meru
    • Halmashauri ya Monduli
    • Halmashauri ya Karatu
    • Halmashauri ya Longido
    • Halmashauri ya Ngorongoro
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo
    • Viwanda
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Ardhi
    • Utalii
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali
    • Habari
    • Matukio

MAAFISA ELIMU ARUSHA WATAKIWA KUFUTILIA WANAFUNZO WALIOPANGIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA 2024....

Posted on: February 14th, 2024

Maafisa Elimu wa halmashauri zote za Mkoa wa Arusha wametakiwa, kuhakikisha kuwa wanafuatilia Wanafunzi wote waliopangiwa kujiunga na kidato cha kwanza ambao hawajaripoti wanaripoti na kuanza masomo kwenye shule waliopangiwa.


Akizungumza wakati akifungua kikao hicho, kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Afisa Elimu mkoa wa Atusha Mwl. Abel Mtupwa,  kikao kazi kilichowakutanishz  Maafisa  Elimu Msingi na Sekondari wa halmashauri, Wathibiti ubora wa shule, Makatibu wasaidizi wa TSC,Viongozi wa TAHOSSA,Wakuu wa shule na Maafisa Elimu kata, kilichofanyika kwenye ukumbi wa Mikutano Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Arusha.


Amewataka viongozi hao wa Elimu kwa nagzi zote, kuwafuatilia wanafunzi waliopangiwa kujiunga na Kidato cha kwanza na hawajaripiti,kuhakikisha wanapata taarifa zao na kama wamehamia shule nyingine ama la na kutoa taarifa zao.


"Serikali imeshafanya maandalizi yote ya kuhakikisha wanafunzi wanakua shuleni kwa wakati, hivyo kila halmashauri ipange mipango yake kupitia Maafisa Elimu kata, watendaji wa kata Vijiji pamoja na Walimu kufuatilia Wanafunzi wote wanaripoti shule wasisubiri agizo la RC au DC la kwenda kuwasaka kwa kuwa mifumo ipo, na kuhakikisha wanafunzi wote wamepatikana" Amsema 


Aidha, amewasisitiza pia kuhakikisha upatikanaji wa chakula shuleni, na kuwataka kuweka mikakati ya wanafunzi kupata chakula cha mchana na kuwasisitiza Mafisa Elimu kufuatilia kwa karibu shule zilizopo kwenye maeneo yao, zinakuwa na mpango wa kutoa chakula kwa Wanafunzi kwa kuwa chakula kinaongeza ufaulu hivyo wakabuni mkakati wa kupatikana chakula.


Ameiagiza halmashauri ichague shule 10 za mfano  na kuhakikisha shule hizo  zinakuwa na ufaulu  uliotukuka na Kila halmashauri ibuni mkakati wa kuhakikisha ufaulu wa mitihani ya taifa  unakuwa ni asilimia 100%.


Kuhusu ,utekelezaji wa miradi ,mkuu huyo wa Mkoa,amezitaka  halmashauri za Wilaya kuhakikisha zinazingatia miongozo ya kukamilisha miradi yote ya Ujenzi  kwa wakati na ubora na Serikali imetoa fedha nyingi za kujenga shule hizo.


Kila halmashauri zihakikishe Elimu inayotolewa ni bora hivyo kila mmoja ajitume awe mkereketwa wa Elimu na awe na maono ya Elimu kwenye eneo lake


 Kuhusu wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza mwaka huu,mkuu wa mkoa,amesema jumla ya Wanafunzi  45908 waliohitimu elimu ya msingi mwaka jana na kupangiwa shule za sekondari za Serikali walioripoti ni 33915 sawa na asimia 74%.


Amesema Mkoa umefanikiwa kutekeleza miradi yote ikiwemo ya fedha za  COVID 19,Boost ,Tozo,Uhuru umekamilika vizuri ,pia Mkoa unatekeleza miradi mwingine ya SEQUIP ,BARRICK bado inaendelea kukamilishwa kwa fedha za  Serikali  


Amesema uandikishaji Wanafunzi darasa la awali umefikia 55414 ,kati ya maoteo ya kuandikisha Wanafunzi 69 174 sawa na asilimia 80 


Aidha uandikishaji darasa la kwanza umefikia 60378 sawa na asilimia 97% kati ya  maoteo ya kuandikisha Wanafunzi 62307.


Kwa upande wake rais wa Umoja wa Wakuu wa shule za Sekondari TAHOSA ,Mwl Denis Otieno ambae pia ni mkuu wa shule ya sekondari Ilboru,amesema Wakuu wa shule wanatekeleza malengo ya Elimu ambapo wanazifanyia kazi changamoto na kuzifanya ziwe ni fursa.


Amesema changamoto iliyopo ni utoro wa wanafunzi hivyo wanashirikiana na Viongozi wa Serikali kuwafuatilia wanafunzi,na kuhamasisha wazazi kuchangia chakula .


Katibu wa TAHOSA mwl Justini Mtongi ,ambae ni mkuu wa shule ya sekondari King'ori,amesema kuwa  mkakati uliopo ni kuzijengea uzoefu shule ambazo hazifanyi vizuri  kwa kuzingatia miongozo mbalimbali


Tangazo

  • TAZAMA MATOKEO YA MTIHANI WA MOCK MKOA DARASA LA SABA 1 July 06, 2023
  • MATOKEO YA MOCK MKOA DARASA LA SABA 2 July 07, 2023
  • TAZAMA MATOKEO YA MOCK MKOA KIDATO CHA NNE July 07, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONDA ASHUHUDIA UTIAJI SAINI UJENZI WA BARABARA YA ESO - LONGDON NA UKUMBI WA MIKUTANO ARUSHA.

    April 03, 2025
  • RC MAKONDA ATAKA KUPEWA MAJINA YA WATENDAJI WANAOCHOCHEA MIGOGORO YA KIJAMII.

    March 28, 2025
  • KAMPENI YA MSAADA WA KISHERIA NI MAONO NA MAELEKEZO YA RAIS SAMIA- WAZIRI NDUMBARO.

    March 28, 2025
  • OFISI YA MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI YAFANYIA KAZI MALALAMIKO WANANCHI WA MIANZINI ARUSHA.

    March 28, 2025
  • Angalia Zote

Video

UZINDUZI WA BARABARA YA WASO-SALE
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • SALARY SLIP
  • Taarifa ya Mapato
  • Taarifa za Shule (SIS)
  • Takwimu za Sekta ya Elimu (BEMIS)
  • Video

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Portal ya Watumishi
  • Takwimu
  • TANAPA

Watembeleaji

world map hits counter

Wasiliana Nasi

Mawaliliano mengine

   

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani
    • Maswali ya Mara kwa Mara

Hatimiliki ©2018 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Arusha. Haki Zote Zimehifadhiwa