Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa amewataka waandishi wa habari nchini kuitumia Akili Mnemba (Artificial Intelligence) kama chombo cha kuwawezesha kutekeleza majukumu yao kwa weledi zaidi, na siyo kama kikwazo cha uhuru wao wa kufanya kazi.
Akizungumza katika Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani 2025 yaliyofanyika kwenye hotel ya Gran Melia jijini Arusha, Waziri Mkuu amesisitiza kuwa teknolojia mpya kama AI inapaswa kupewa nafasi katika tasnia ya habari ili kuongeza ubunifu, ufanisi na kufikia jamii kwa haraka zaidi.
Aidha, Katika hotuba yake, ametoa wito kwa wanahabari kuendelea Kudumisha maadili ya utangazaji na uandishi wa habari , Kufanya kazi kwa kuzingatia sheria na taratibu za nchi, Kutoa taarifa zinazojenga jamii na kuleta matokeo chanya Pamoja na Kutangaza mafanikio ya serikali kwa uwazi na uadilifu
Ameongeza kuwa uhuru wa vyombo vya habari lazima ulindwe, huku akisisitiza kuwa hakuna uhuru usio na mipaka – ukizingatia maslahi mapana ya taifa.
maadhimisho hayo yameambatana na kaulimbiu isemayo "Uhabarishaji kwenye dunia mpya: Mchango wa Akili Unde kwenye uhuru wa vyombo vya Habari"
Hatimiliki ©2018 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Arusha. Haki Zote Zimehifadhiwa