• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Arusha Regional

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Mkoa
      • Chimbuko/Asili ya eneo
      • Orodha ya wakuu wa Mikoa
    • Dira na dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji Mali
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Wilaya
    • Arusha
      • Historia
      • Viongozi
    • Arumeru
      • Historia
      • Viongozi
    • Monduli
      • Historia
      • Viongozi
    • Karatu
      • Historia
      • Viongozi
    • Longido
      • Historia
      • Viongozi
    • Ngorongoro
      • Historia
      • Viongozi
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Arusha
    • Halmashauri ya Arusha
    • Halmashauri ya Meru
    • Halmashauri ya Monduli
    • Halmashauri ya Karatu
    • Halmashauri ya Longido
    • Halmashauri ya Ngorongoro
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo
    • Viwanda
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Ardhi
    • Utalii
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali
    • Habari
    • Matukio

ONGEZENI UFAULU WA SHULE ZA MSINGI-RC KIMANTA

Posted on: April 19th, 2021

Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. Iddi Hassan Kimanta amewaagiza wakurugenzi na Maafisa elimu Mkoa wa Arusha kuhakikisha ufaulu unaongezeka katika shule zote za Msingi.

Maelekezo hayo ameyatoa alipokuwa akizindua miradi mbalimbali katika shule ya msingi Endabash wilayani Karatu, miradi iliyofadhiriwa na shirika la World Vision Tanzania.

Amesema ni aibu kubwa kwa shule kama ile kupata majengo mazuri ya Madarasa,Ofisi ya walimu, Madawati na Vyoo alafu ufaulu uwe chini kwani kwa mwaka jana 2020 ulikuwa 67%.

Kimanta amesema mwaka jana 2020 ufaulu wa Mkoa kwa shule za msingi ulikuwa 92.4%, hivyo kwa mwaka huu 2021 anataka kila shule ifaulishe si chini ya 90% ili kurudisha fadhila zinazotolewa na wafadhili hao na kuendelea kuwatia moyo ili waongeze miradi mingine mingi.

Hata hivyo, Kimanta amewasisitiza wazazi kutoa ushirikiano katika juhudi hizo kwa kusimamia mahudhuria ya Watoto wao kwa kuwahimiza kuhudhuria shule kila mara.

Pia, amewataka wananchi wa Kijiji cha Endabash kuwaunga mkono wadau hao wa maendeleo kwa kujenga bwalo la chakula kwani shule hiyo haina bwalo la chakula ambalo inaleta usumbufu kwa Watoto kukosa sehemu ya kupatia chakula hasa katika kipindi cha mvua.

Nae,Kaimu Mkurugenzi wa Mradi kutoka World Vison bwana Victor Kasabala, amesema shirika hilo limekuwa likifanya kazi katika Mikoa takribani 16 hapa Tanzania na wamejikita katika sekta mbalimbali ikiwemo Elimu, Afya, Maji na kukuza ufahamu kwa wasichana.

Amesema, shirika hilo limeweza kutekeleza miradi yake kwa urahisi kutokana na mazingira mazuri yalipo ya Amani na Utulivyo yaliyotengenezwa na Serikali ya Tanzania.

Meneja Mradi kutoka World Vision bwana Goodluck Nnko amesema, mradi huo ulikuwa wa kujenga Madarasa 10, jengo moja la utawala, Matundu ya Vyoo 18, Madawati 66, Masinki vituo 3 na Jiko.

Mradi huo ilianza July 2020 na umekamilika Aprili 2021 na jumla ya Shilingi Milioni 558 zimetumika katika mradi huo.

Bwana Nnko amesema, World Vision wanaendelea kushirikiana na Serikali katika kuleta maendeleo kwenye nyanja mbalimbali kama vile sekta ya Maji, Afya na Elimu.

Shirika la World Vision Tanzania limekabidhi jumla ya miradi 7 kwa Serikali baada ya kukamilika katika shule ya msingi Endabash na wanaendelea kusimamia miradi mingine katika halmashauri mbalimbali za Mkoa wa Arusha.

Tangazo

  • TAZAMA MATOKEO YA MTIHANI WA MOCK MKOA DARASA LA SABA 1 July 06, 2023
  • MATOKEO YA MOCK MKOA DARASA LA SABA 2 July 07, 2023
  • TAZAMA MATOKEO YA MOCK MKOA KIDATO CHA NNE July 07, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONDA ASHUHUDIA UTIAJI SAINI UJENZI WA BARABARA YA ESO - LONGDON NA UKUMBI WA MIKUTANO ARUSHA.

    April 03, 2025
  • RC MAKONDA ATAKA KUPEWA MAJINA YA WATENDAJI WANAOCHOCHEA MIGOGORO YA KIJAMII.

    March 28, 2025
  • KAMPENI YA MSAADA WA KISHERIA NI MAONO NA MAELEKEZO YA RAIS SAMIA- WAZIRI NDUMBARO.

    March 28, 2025
  • OFISI YA MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI YAFANYIA KAZI MALALAMIKO WANANCHI WA MIANZINI ARUSHA.

    March 28, 2025
  • Angalia Zote

Video

UZINDUZI WA BARABARA YA WASO-SALE
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • SALARY SLIP
  • Taarifa ya Mapato
  • Taarifa za Shule (SIS)
  • Takwimu za Sekta ya Elimu (BEMIS)
  • Video

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Portal ya Watumishi
  • Takwimu
  • TANAPA

Watembeleaji

world map hits counter

Wasiliana Nasi

Mawaliliano mengine

   

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani
    • Maswali ya Mara kwa Mara

Hatimiliki ©2018 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Arusha. Haki Zote Zimehifadhiwa