• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Arusha Regional

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Mkoa
      • Chimbuko/Asili ya eneo
      • Orodha ya wakuu wa Mikoa
    • Dira na dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji Mali
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Wilaya
    • Arusha
      • Historia
      • Viongozi
    • Arumeru
      • Historia
      • Viongozi
    • Monduli
      • Historia
      • Viongozi
    • Karatu
      • Historia
      • Viongozi
    • Longido
      • Historia
      • Viongozi
    • Ngorongoro
      • Historia
      • Viongozi
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Arusha
    • Halmashauri ya Arusha
    • Halmashauri ya Meru
    • Halmashauri ya Monduli
    • Halmashauri ya Karatu
    • Halmashauri ya Longido
    • Halmashauri ya Ngorongoro
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo
    • Viwanda
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Ardhi
    • Utalii
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali
    • Habari
    • Matukio

RC MAKONDA AKERWA NA TABIA YA WATENDAJI KUTOTEMBELEA MIRADI YA MAENDELEO....

Posted on: May 23rd, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. Paul Christian Makonda ameonya tabia ya baadhi ya watendaji wa serikali na taasisi zake kutotembelea miradi ya maendeleo suala ambalo limekuwa likisababisha wananchi kuteseka ma ukosefu wa huduma mbalimbali za kijamii licha ya serikali kutoa fedha nyingi za kutekeleza miradi hiyo.


Mkuu wa Mkoa Mhe. Paul Christian Makonda ametoa kauli hiyo mapema leo Mei 23, 2024 wakati alipotembelea Zahanati ya Kijiji cha Lemereta pembezoni mwa Mji wa Longido na kuelezwa kuhusu changamoto za ukosefu wa Umeme wa Uhakika na kutopatikana kwa maji kwenye zahanati hiyo iliyo muhimu kwa wakazi wa Kijiji cha Lemereta.


Bwana Supuk Melita Mwenyekiti wa kijiji cha Lemereta amemueleza Mhe. Mkuu wa Mkoa kwamba licha ya kutoa taarifa kwa Mamlaka ya Maji vijijini na kwa Shirika la Umeme Tanesco Wilaya ya Longido, ni miezi mitatu sasa hawakuwahi kuona maafisa wa mamlaka hizo wakifika na kutatua changamoto walizowasilishiwa na wananchi.


Kufuatia hali hiyo, Mhe. Mkuu wa Mkoa amemtaka Bwana Ramadhan Musiba, Meneja wa Mamlaka ya Maji vijijini Wilaya ya Longido kumuandikia barua mteule wake (Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji) ili kueleza kuhusu udanganyifu alioutoa kwa Uongozi wa Mkoa pamoja na kushindwa kuwa mfuatiliaji mzuri wa miradi ya Maji inayotakiwa kusimamia na ofisi yake.


Katika Hatua nyingine Mhe. Makonda amemuagiza Bwana Lazaro Lenoi, Meneja wa Tanesco Wilaya ya Longido kuhakikisha kuwa ndani ya siku tatu Zahanati ya Lemereta inakuwa na Umeme wa kutosha ili kuondokana na changamoto ya Umeme kushindwa kuendesha vifaatiba na mashine nyingine zinazotumika kwenye Zahanati hiyo.


Mhe. Makonda amewataka watendaji kuwa na utamaduni wa kwenda kwa wananchi kila wakati na kutatua changamoto zao badala ya kukaa ofisini pekee na matokeo yake kusababisha ubadhirifu, uharibifu na kusuasua kwa miradi mingi ya maendeleo inayosimamiwa na serikali ya awamu ya sita.

Tangazo

  • TAZAMA MATOKEO YA MTIHANI WA MOCK MKOA DARASA LA SABA 1 July 06, 2023
  • MATOKEO YA MOCK MKOA DARASA LA SABA 2 July 07, 2023
  • TAZAMA MATOKEO YA MOCK MKOA KIDATO CHA NNE July 07, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONDA ASHUHUDIA UTIAJI SAINI UJENZI WA BARABARA YA ESO - LONGDON NA UKUMBI WA MIKUTANO ARUSHA.

    April 03, 2025
  • RC MAKONDA ATAKA KUPEWA MAJINA YA WATENDAJI WANAOCHOCHEA MIGOGORO YA KIJAMII.

    March 28, 2025
  • KAMPENI YA MSAADA WA KISHERIA NI MAONO NA MAELEKEZO YA RAIS SAMIA- WAZIRI NDUMBARO.

    March 28, 2025
  • OFISI YA MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI YAFANYIA KAZI MALALAMIKO WANANCHI WA MIANZINI ARUSHA.

    March 28, 2025
  • Angalia Zote

Video

UZINDUZI WA BARABARA YA WASO-SALE
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • SALARY SLIP
  • Taarifa ya Mapato
  • Taarifa za Shule (SIS)
  • Takwimu za Sekta ya Elimu (BEMIS)
  • Video

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Portal ya Watumishi
  • Takwimu
  • TANAPA

Watembeleaji

world map hits counter

Wasiliana Nasi

Mawaliliano mengine

   

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani
    • Maswali ya Mara kwa Mara

Hatimiliki ©2018 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Arusha. Haki Zote Zimehifadhiwa