• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Arusha Regional

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Mkoa
      • Chimbuko/Asili ya eneo
      • Orodha ya wakuu wa Mikoa
    • Dira na dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji Mali
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Wilaya
    • Arusha
      • Historia
      • Viongozi
    • Arumeru
      • Historia
      • Viongozi
    • Monduli
      • Historia
      • Viongozi
    • Karatu
      • Historia
      • Viongozi
    • Longido
      • Historia
      • Viongozi
    • Ngorongoro
      • Historia
      • Viongozi
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Arusha
    • Halmashauri ya Arusha
    • Halmashauri ya Meru
    • Halmashauri ya Monduli
    • Halmashauri ya Karatu
    • Halmashauri ya Longido
    • Halmashauri ya Ngorongoro
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo
    • Viwanda
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Ardhi
    • Utalii
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali
    • Habari
    • Matukio

RC MONGELLA AKAGUA MRADI WA KITIVO CHA TEKNOLOJIA ZA KIHANDISI (KITEKI) GONGALI - KARATU..

Posted on: December 1st, 2023

Na Elinipa Lupembe


Mkuu wa mkoa wa Arusha Mhe. John V.K Mongella, ametembelea mradi wa Kitovu cha Teknolojia za Kihandisi (KITEKI) Kijiji cha Gongali wilaya ya Karatu, mradi uliogharimu shilingi milioni 450.9 huku wananchi wa kijiji hicho, wakitoa eneo lenye ukubwa wa Ekari 3.


Mhe. Mongella licha ya kupongeza utekelezaji wa mradi huo, amewataka KITEKI, kutoa mafunzo kwa wakulima ya namna bora ya matumizi ya mashine hizo, huku akiwasisitiza kuuza na kukodisha mashine hizo kwa bei ambayo ni nafuu ili wakulima wote waweze kumudu kutumia zana hizo.


Amesema kuwa serikali ya awamu ya sita, imejipanga kwawawezesha wananchi kujikwamua kiuchumi ili kukabiliana na uhaba wa ajira pamoja na kuhakikisha huduma muhimu za jamii zinakuwa karibu na wananchi kulingana na mahitaji na vipaumbele.


"Tumeni kituo hiki kama sehemu ya kujifunza na kujipatia zana za kilimo na mifugo kwa bei nafuu, Serikali ya mama Samia, inataka kila mwananchi ajikite katika kufanya kazi za uzalishaji ili kukuza uchumi wa Taifa, Kupitia kituo hiki, muungeni mkono mama Samia kwa kufanya kazi kwa bidii" Amesisitiza Mhe. Mongella


Serikali imeanzisha mradi huo kwa lengo la kusogeza huduma karibu na wakulima na wafugaji, kurahisisha upatikanaji wa huduma za teknolojia za kihandisi hususani zana za kilimo, ufugaji, uvuvi ili kuongeza matumizi ya zana hizo na kuongeza tija katika sekta ya kilimo.


Uwepo wa Teknolojia hizo karibu na wakulima, kutachangia ongezeko la uzalishaji wa mazao ya chakula na malighafi muhimu kwa ajili ya viwanda vidogo, ili kuboresha kipato na ustawi wa jamii pamoja na kutengeneza ajira kwa vijana na wanawake nchini.


Hata hivyo, kituo hicho kitatoa huduma za uuzaji na ukodishaji wa mashine, kutoa mafunzo juu ya matumizi sahihi ya mashine kwa ajili ya kutatua changamoto katika sekta ya kilimo na mifugo pamoja na kuwa chanzo cha taarifa muhimu kwa wabunifu na kuwa chanzo cha upatikanaji wa mashine muhimu zinazotengenzwa nchini.


Tangazo

  • TAZAMA MATOKEO YA MTIHANI WA MOCK MKOA DARASA LA SABA 1 July 06, 2023
  • MATOKEO YA MOCK MKOA DARASA LA SABA 2 July 07, 2023
  • TAZAMA MATOKEO YA MOCK MKOA KIDATO CHA NNE July 07, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONDA ASHUHUDIA UTIAJI SAINI UJENZI WA BARABARA YA ESO - LONGDON NA UKUMBI WA MIKUTANO ARUSHA.

    April 03, 2025
  • RC MAKONDA ATAKA KUPEWA MAJINA YA WATENDAJI WANAOCHOCHEA MIGOGORO YA KIJAMII.

    March 28, 2025
  • KAMPENI YA MSAADA WA KISHERIA NI MAONO NA MAELEKEZO YA RAIS SAMIA- WAZIRI NDUMBARO.

    March 28, 2025
  • OFISI YA MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI YAFANYIA KAZI MALALAMIKO WANANCHI WA MIANZINI ARUSHA.

    March 28, 2025
  • Angalia Zote

Video

UZINDUZI WA BARABARA YA WASO-SALE
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • SALARY SLIP
  • Taarifa ya Mapato
  • Taarifa za Shule (SIS)
  • Takwimu za Sekta ya Elimu (BEMIS)
  • Video

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Portal ya Watumishi
  • Takwimu
  • TANAPA

Watembeleaji

world map hits counter

Wasiliana Nasi

Mawaliliano mengine

   

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani
    • Maswali ya Mara kwa Mara

Hatimiliki ©2018 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Arusha. Haki Zote Zimehifadhiwa