• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Arusha Regional

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Mkoa
      • Chimbuko/Asili ya eneo
      • Orodha ya wakuu wa Mikoa
    • Dira na dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji Mali
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Wilaya
    • Arusha
      • Historia
      • Viongozi
    • Arumeru
      • Historia
      • Viongozi
    • Monduli
      • Historia
      • Viongozi
    • Karatu
      • Historia
      • Viongozi
    • Longido
      • Historia
      • Viongozi
    • Ngorongoro
      • Historia
      • Viongozi
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Arusha
    • Halmashauri ya Arusha
    • Halmashauri ya Meru
    • Halmashauri ya Monduli
    • Halmashauri ya Karatu
    • Halmashauri ya Longido
    • Halmashauri ya Ngorongoro
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo
    • Viwanda
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Ardhi
    • Utalii
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali
    • Habari
    • Matukio

RC MONGELLA: KUTOA NI MOYO SIO UTAJIRI; CHAMA CHA ACRO ARUSHA WAKABIDHI MSAADA KWA WAHANGA MAAFA KATESH

Posted on: December 20th, 2023

Na Elinipa Lupembe


Ule usemi unaosema Kutoa ni moyo na sio utajiri, umejithihirisha leo, kwa Wanachama wa Chama cha Kutetea Haki za Watoto wanaoishi kwenye Makazi mkoa wa Arusha ( ACRO), kwa kukabidhi msaada wa vitu mbalimbali kwa Waathirika wa Maafa ya Katesh wilaya ya Hanang.


Usemi huo umethibitishwa na Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mhe. John V.K Mongella, mara baada ya kukabidhiwa msaada huo, uliotolewa na wanachama hao, ambao wao pia, hushughulika na kusaidia watoto wanaoishi kwenye makao ya kukulea watoto wenye uhitaji.


Mhe. Mongella licha ya kuwashukuru kwa moyo wa utoaji walionao, amekiri kushangazwa na Chama hicho, kutokana na ukweli kuwa, wao pia wanafanya shughuli za kuwasidia jamii yenye uhitaji pia lakini bado wameguswa kutoa kwa wengine wenye uhitaji zaidi.


"Mara nyingi tulizoea wakipita kutaka kushikwa mkono kwa ajili ya kuwasiaidia watoto wanaoishi kwenye mazingira magumu, leo wao wanatoa msaada kwa waathirika wa Maafa ya Katesh, hili jambo limenidhihirishia kweli kutoa sio utajiri bali ni moyo" Amethibitisha Mhe. Mongella.


Aidha amewataka wakazi wa mkoa wa Arusha, watakao guswa kutoa msaada wafanye hivyo, kwa kuwa bado wenzetu wanaKatesh wanahitaji msaada, kazi ya mkoa ni kuratibu na kuhakikisha misaada yote inayotolewa, inawafikia walengwa na si vinginevyo, kama yalivyo maagizo ya Serikali chini ya Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan.


"Tumeelekezwa na Mhe. Rais kuratibu zoezi la upokeaji misaada na kuifikisha kwa waathirika, nitamfikishia salaam za wana ACRO, tendo hili ni funzo kwetu na watanzania wote, tunapaswa kuiga mfano huu, hata hivyo fedha mlizotoa kwa ajili ya kusafirishia mzigo huu, tutaziwasilisha kwa walengwa kwa kuwa hilo ni jukumu la mkoa kusafirisha misaada itakayotolewa kwa waathirika wa Katesh" Amebainisha Mkuu huyo wa mkoa.


Akikabidhi msaada huo, Mwenyekiti wa Chama cha ACRO, Josephat Mmanyi, amesema wameguswa kutoa msaada wa vifaa hivyo ikiwemo, vyakula, nguo na mashuka, kwa lengo la kuuwasaidia watanzania wenzao wenye shida pamoja na kuunga mkono mhe. Rais Dkt Samia Suluhu pamoja na mkuu wa mkoa wa Arusha.


"Tumeguswa kuwasaidia watu wa Hanang' waliokumbwa na maafa, ili waweze kujiona wapo na ndugu zao, ambao ni sisi watanzania wenzao, tunawaomba wakazi wa Arusha kumuunga mkono mkuu wa mkoa ili wenzetu waweze kupata huduma kama ilivyokuwa awali.


Naye, Afisa Ustawi wa Jamii, Mkoa wa Arusha, Denis Mgie, ameshukuru wadau hao kwa msaada huo kwa kuwa wapo watoto ambao wameathirika katika eneo la Katesh, hivyo msaada huo utakwenda kuwahudumia watoto pia waliokumbwa na maafa hayo.


Tangazo

  • TAZAMA MATOKEO YA MTIHANI WA MOCK MKOA DARASA LA SABA 1 July 06, 2023
  • MATOKEO YA MOCK MKOA DARASA LA SABA 2 July 07, 2023
  • TAZAMA MATOKEO YA MOCK MKOA KIDATO CHA NNE July 07, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONDA ASHUHUDIA UTIAJI SAINI UJENZI WA BARABARA YA ESO - LONGDON NA UKUMBI WA MIKUTANO ARUSHA.

    April 03, 2025
  • RC MAKONDA ATAKA KUPEWA MAJINA YA WATENDAJI WANAOCHOCHEA MIGOGORO YA KIJAMII.

    March 28, 2025
  • KAMPENI YA MSAADA WA KISHERIA NI MAONO NA MAELEKEZO YA RAIS SAMIA- WAZIRI NDUMBARO.

    March 28, 2025
  • OFISI YA MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI YAFANYIA KAZI MALALAMIKO WANANCHI WA MIANZINI ARUSHA.

    March 28, 2025
  • Angalia Zote

Video

UZINDUZI WA BARABARA YA WASO-SALE
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • SALARY SLIP
  • Taarifa ya Mapato
  • Taarifa za Shule (SIS)
  • Takwimu za Sekta ya Elimu (BEMIS)
  • Video

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Portal ya Watumishi
  • Takwimu
  • TANAPA

Watembeleaji

world map hits counter

Wasiliana Nasi

Mawaliliano mengine

   

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani
    • Maswali ya Mara kwa Mara

Hatimiliki ©2018 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Arusha. Haki Zote Zimehifadhiwa