• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Arusha Regional

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Mkoa
      • Chimbuko/Asili ya eneo
      • Orodha ya wakuu wa Mikoa
    • Dira na dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji Mali
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Wilaya
    • Arusha
      • Historia
      • Viongozi
    • Arumeru
      • Historia
      • Viongozi
    • Monduli
      • Historia
      • Viongozi
    • Karatu
      • Historia
      • Viongozi
    • Longido
      • Historia
      • Viongozi
    • Ngorongoro
      • Historia
      • Viongozi
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Arusha
    • Halmashauri ya Arusha
    • Halmashauri ya Meru
    • Halmashauri ya Monduli
    • Halmashauri ya Karatu
    • Halmashauri ya Longido
    • Halmashauri ya Ngorongoro
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo
    • Viwanda
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Ardhi
    • Utalii
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali
    • Habari
    • Matukio

TAASISI ZA ULINZI ARUSHA ZATAKIWA KUSHIRIKIANA NA WANAHABARI

Posted on: July 11th, 2024


Na Elinipa Lupembe


Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mhe. Paul Christian Makonda amezitaka Taasisi za Ulinzi Arusha kushirikiana na waandishi wa habari ili wapate taarifa muhimu kuhusu Taasisi zao na mambo yanayoendelea kwenye Taasisi hizo.


Mhe. Makonda amesema hayo, kwenye kikao kazi kilichowakutanisha Wakuu wa Taasisi za Ulinzi mkoa wa Arusha, ikiwepo Jeshi la Polisi, TAKUKURU,Jeshi la Zimamoto, Uhamiaji, Taasisi ya kupambana na Dawa za Kulevya, kilichofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano Ofisi ya Mkuu wa mkoa huo, Julai, 11,2024.


Amefafanua kuwa upo umuhimu wa taasisi hizo, kushirikiana na waandishi wa habari, kwa kuwa na utaratibu wa kutoa taarifa kwa waandishi wa habari kuhusu taasisi zao na mambo yanayoendelea kuliko kusubiri kuona taarifa kwenye vyomba vya habari, taarifa ambazo hazina uhalisia.


Uchumi wa mkoa wa Arusha, unategemea sana ujio wa watalii kutoka ndani na nje ya nchi, uwepo wa taarifa zisizo na uhalisia licha ya kuharibu taswira ya mkoa, zinaharibu taswira ya nchi sambamba na kuharibu soko la utalii, soko ambalo ni tegemeo la mkoa na Taifa.


"Ninatamani wakuu wa Taasisi za Ulinzi kuwa na mahusiano mazuri na waandishi wa habari na vyombo vya habari kwa kuwapa taarifa, ili kuwa na uelewa wa pamoja utakaowezesha wananchi kupata taarifa sahihi kutoka kwenye vyanzo sahihi, hali hii itaondoa taharuki za mara kwa mara". Amesisitiza Mhe. Makonda.


Zipo taarifa ambazo zinatolewa na vyombo vya habari, taarifa ambazo hazina uhalisia na kusababisha taharuki kwa wananchi na wageni, upo umuhimu wa kuwa na vyanzo sahihi vya taarifa za mkoa wa Arusha, taarifa ambazo zitajenga heshima ya mkoa na Taifa kwa ujumla wake.


"Ili kuondoa taarifa zinazozua taharuki na sintofahamu kwa wananchi, ni muhimu kuwa na utaratibu wa kuwapa taarifa sahihi  wanahabari, wananchi watapata taarifa sahihi, hivyo ni vema  vyombo vya usalama vikatoka taarifa kwa uŕahisi ili wananchi wazifahamu, zaidi zitauletea sifa ya mkoa wetu, mkoa ambao una wageni wengi wa ndani na nje ya nchi.


Hata hivyo, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, SACP Justine Masejo, amewataka waandishi wa habari kuweka uzalendo mbele kabla ya kutoa habari jambo ambalo litaweka utaifa mbele badala ya maslahi binafsi.


"Ni muhimu vyombo vya habari kuweka maslahi ya Taifa mbele, hakuna maana ya kulipaka matope Taifa letu kwa 'interest' za muda mfupi, tuangalie uwepo wa vita ya kiuchumi duniani" Amesema Kamanda Masejo.


Tangazo

  • TAZAMA MATOKEO YA MTIHANI WA MOCK MKOA DARASA LA SABA 1 July 06, 2023
  • MATOKEO YA MOCK MKOA DARASA LA SABA 2 July 07, 2023
  • TAZAMA MATOKEO YA MOCK MKOA KIDATO CHA NNE July 07, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONDA ASHUHUDIA UTIAJI SAINI UJENZI WA BARABARA YA ESO - LONGDON NA UKUMBI WA MIKUTANO ARUSHA.

    April 03, 2025
  • RC MAKONDA ATAKA KUPEWA MAJINA YA WATENDAJI WANAOCHOCHEA MIGOGORO YA KIJAMII.

    March 28, 2025
  • KAMPENI YA MSAADA WA KISHERIA NI MAONO NA MAELEKEZO YA RAIS SAMIA- WAZIRI NDUMBARO.

    March 28, 2025
  • OFISI YA MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI YAFANYIA KAZI MALALAMIKO WANANCHI WA MIANZINI ARUSHA.

    March 28, 2025
  • Angalia Zote

Video

UZINDUZI WA BARABARA YA WASO-SALE
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • SALARY SLIP
  • Taarifa ya Mapato
  • Taarifa za Shule (SIS)
  • Takwimu za Sekta ya Elimu (BEMIS)
  • Video

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Portal ya Watumishi
  • Takwimu
  • TANAPA

Watembeleaji

world map hits counter

Wasiliana Nasi

Mawaliliano mengine

   

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani
    • Maswali ya Mara kwa Mara

Hatimiliki ©2018 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Arusha. Haki Zote Zimehifadhiwa