• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Arusha Regional

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Mkoa
      • Chimbuko/Asili ya eneo
      • Orodha ya wakuu wa Mikoa
    • Dira na dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji Mali
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Wilaya
    • Arusha
      • Historia
      • Viongozi
    • Arumeru
      • Historia
      • Viongozi
    • Monduli
      • Historia
      • Viongozi
    • Karatu
      • Historia
      • Viongozi
    • Longido
      • Historia
      • Viongozi
    • Ngorongoro
      • Historia
      • Viongozi
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Arusha
    • Halmashauri ya Arusha
    • Halmashauri ya Meru
    • Halmashauri ya Monduli
    • Halmashauri ya Karatu
    • Halmashauri ya Longido
    • Halmashauri ya Ngorongoro
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo
    • Viwanda
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Ardhi
    • Utalii
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali
    • Habari
    • Matukio

TUMIENI FEDHA ZA MIRADI KAMA ZILIVYOPANGWA

Posted on: November 19th, 2021


Katibu Tawala Mkoa wa Arusha Dkt Athumani Kihamia amesema wilaya ya Longido ni moja ya wilaya iliyopewa fedha nyingi kwa ajili ya ujenzi wa shule shikizi kutokana na Jiografia ya eneo hilo,na kutoa wito kwa wasimamizi wa ujenzi kutofanya ubadhirifu wa fedha hizo.

Dkt Kihamia alisema wilaya hiyo imepewa sh billion 1 kwa ajili ya ujenzi wa Madarasa 50 maeneo mbalimbali katika wilaya,fedha hizi ni za moto msijaribu kuzitumia kinyume na kile kilichoagizwa.

Akizungumzia hali ya miradi inavyotekelezwa ,alisema pamoja na kuwa wilaya hiyo upatikanaji wa Nyenzo(Material) kwa ajili ya ujenzi ni changamoto lakini viongozi wamejitahidi kusimamia tofauti na maeneo mengine ambayo malighafi zinapatikana kwa haraka.

" Mmejitahidi na mpo kwenye hatua nzuri,lakini haimaanishi kuwa mmeshamaliza kazi, bado tutarudi kukagua na wataendelea kuja watu kutoka maeneo mbalimbali kwa ajili ya kukagua miradi hii ikiwemo TAKUKURU"Alisema Dkt Kihamia.

Katika hatua nyingine,aliwahasa wazazi kuwapeleka watoto shule na kuachana na desturi ya kuwachungisha mifugo,kwani serikali inatambua haki ya elimu kwa mtoto ndio maana Rais Samia ametoa fedha za ujenzi wa Madarasa hayo na kuwasogezea huduma karibu watoto wasiendelee kutembea umbali mrefu kufuata elimu.

Jacob Laizer Mkazi wa Kata ya Orbomba Tarafa ya Longido akizungumza kwa niaba ya wananchi alitoa shukrani kwa Rais Samia kwa kuleta fedha za miradi ya elimu na kudai kuwa shule nyingi wilayani humo zenye ufaulu duni wa watoto ni kutokana na umbali mrefu wa kwenda shule.

Alisema,uwepo wa shule hizo karibu na jamii kutasaidia kupunguza kuzorota kwa elimu kwa watoto wa jamii ya kifugaji,kwani Uvivu wa kutembea zaidi ya kilomita 10_25 kufuata elimu utapungua na watoto watasoma kwa raha.

" Hata hivyo watoto wetu walipokua wakitembea umbali mrefu kufuata elimu kwenye shule mama za msingi walikua wakikutana na wanyama wakali hali hiyo pia ilikua ikiwatia hofu na kukata tamaa ya kuendelea na masomo na kupeleka utoro sugu wa wanafunzi" alidai Laizer.

Hata hivyo Mkuu wa Wilaya Nurudin Babu katika ziara yake aliwasisitiza jamii hiyo kutumia majengo hayo pindi yatakapo kamilika  kwa kuhakikisha watoto wanakwenda shule ili yasibaki kama Ghofu na nyumba ya wadudu Kama vile Buibui.

Aidha aliwataka jamii kujiongeza kwa ajili ya ujenzi wa vyoo katika maeneo yaliyojengwa shule shikizi sambamba na Madarasa hayo ili watoto watakapoanza kusoma wapate huduma ya vyoo na kuepuka kujisaidia maeneo yasiyorasmi Mfano vichakani.

" Naomba acheni tabia ya kuwakeketa watoto wakike pamoja na ndoa za utotoni" aliomba Babu.

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Longido Stephen Ulaya alisema pamoja na kuwepo kwa changamoto ya upatikanaji wa maji na matofali,lakini wamejipanga kukabiliana nalo na ifikapo Desemba 15 Madarasa hayo yatakua yamekamilika.

Ikumbukwe kuwa fedha hizi ni fedha za Mpango wa serikali ya Tanzania wa kuinua Uchumi kwa kutumia mkopo wa fedha wa Sh. Trillion 1.3 uliotolewa na shirika la fedha Duniani (IMF) na kukabiliana na ugonjwa wa Virusi vya Korona (UVIKO 19).



Tangazo

  • TAZAMA MATOKEO YA MTIHANI WA MOCK MKOA DARASA LA SABA 1 July 06, 2023
  • MATOKEO YA MOCK MKOA DARASA LA SABA 2 July 07, 2023
  • TAZAMA MATOKEO YA MOCK MKOA KIDATO CHA NNE July 07, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONDA AFUNGUA MKUTANO WA 33 WA WAKUU WA MAJESHI YA ULINZI (SADC).

    May 30, 2025
  • SAMIA MOTOCROSS CHAMPIONSHIP KUREJEA MSIMU WA PILI JULAI 12, 2025

    May 27, 2025
  • MKOA WA ARUSHA KUWA MWENYEJI WA MKUTANO MKUBWA WA WAKUU WA MAJESHI WA SADC

    May 25, 2025
  • UJENZI WA UWANJA WA AFCON ARUSHA SIO MICHEZO TU, NI FURSA YA KIUCHUMI

    May 24, 2025
  • Angalia Zote

Video

UZINDUZI WA BARABARA YA WASO-SALE
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • SALARY SLIP
  • Taarifa ya Mapato
  • Taarifa za Shule (SIS)
  • Takwimu za Sekta ya Elimu (BEMIS)
  • Video

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Portal ya Watumishi
  • Takwimu
  • TANAPA

Watembeleaji

world map hits counter

Wasiliana Nasi

Mawaliliano mengine

   

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani
    • Maswali ya Mara kwa Mara

Hatimiliki ©2018 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Arusha. Haki Zote Zimehifadhiwa