• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Arusha Regional

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Mkoa
      • Chimbuko/Asili ya eneo
      • Orodha ya wakuu wa Mikoa
    • Dira na dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji Mali
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Wilaya
    • Arusha
      • Historia
      • Viongozi
    • Arumeru
      • Historia
      • Viongozi
    • Monduli
      • Historia
      • Viongozi
    • Karatu
      • Historia
      • Viongozi
    • Longido
      • Historia
      • Viongozi
    • Ngorongoro
      • Historia
      • Viongozi
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Arusha
    • Halmashauri ya Arusha
    • Halmashauri ya Meru
    • Halmashauri ya Monduli
    • Halmashauri ya Karatu
    • Halmashauri ya Longido
    • Halmashauri ya Ngorongoro
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo
    • Viwanda
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Ardhi
    • Utalii
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali
    • Habari
    • Matukio

WADAU WA MAENDELEO WATAKIWA KUWEKA WAZI GHARAMA ZA FEDHA ZA SHUGHULI ZA MAENDELEO WANAZOZIFANYA.

Posted on: August 9th, 2024

Na Elinipa Lupembe 


Wadau wa Maendeleo Mkoa wa Arusha, wamesisitizwa kuweka wazi taarifa za fedha zinazotumika katika kutekeleza shughuli za maendeleo ikiwemo utekelezaji wa miradi ya maendeleo katika maeneo yote ya mkoa wa Arusha.


Rai hiyo imetolewa na Katibu Tawala Mkoa wa Arusha na Mwenyekiti wa Kikao, Missaile Albano Musa, wakati wa kikao cha Kamati ya Lishe Mkoa cha mwezi Januari -Juni, 2024, kilichofanyika kwenye Ofisi ya Katibu Tawala huyo, Agosti 09, 2024.


Missaile amewakumbusha wadau wa maendeleo na Mashirika yasiyo ya kiserikali kufanya shughuli zao, kwa kuzingatia kanuni, sheria na taratibu za Serikali,  ikiwemo uwazi wa matumizi ya fedha zinazotumika kutekeleza shughuli za kijamii na miradi ya maendeleo.


"Kila ASAS inawajibika kuweka wazi miradi inayotekelezwa na gharama zake kwenye eneo husika, kuwasilisha taarifa za utekelezaji kwa mamlaka za Serikali za Mitaa, hali ambayo licha ya kuongeza uwazi, uwajibikaji na ufanisi wenye tija kwa jamii, zaidi inaiwezesha Serikali kutambua kazi na huduma zinazotolewa kwa wananchi kupitia mashirika hayo yasiyo ya kiserikali". Amesema Missaile


Aidha, amebainisha kuwa, Serikali inatambua na kuthamini kazi kubwa inayofanywa na Mashirika yasiyo ya kiserikali nchini, wadau ambao wanaisaidia Serikali, kufika malengo yake ya kuhudumia jamii kisekta  pamoja na kusukuma gurudumu la maendeleo la Taifa la Tanzania.


"Tunatambua na kuthamini kazi kubwa inayofanywa na mashirika ya kiraia, kazi ambayo inatoa mchango mkubwa kwa jamii kwa niaba ya Serikali, mchango ambao wakati mwingine Serikali peke yake isingeweza, hivyo Asas zote za kiraia ziendelee kutekeleza majukumu yake kwa kuzingatia taratibu na mpango mkakati wa Serikali" Amesema


Kikao hicho cha lishe kinajumuisha wajumbe wa idara mtambuka za Lishe, ikiwemo Elimu,Afya, mipango pamoja na wadau wa lishe kutoka mashirika yasiyo ya kiserikali mkoa wa Arusha.


Tangazo

  • TAZAMA MATOKEO YA MTIHANI WA MOCK MKOA DARASA LA SABA 1 July 06, 2023
  • MATOKEO YA MOCK MKOA DARASA LA SABA 2 July 07, 2023
  • TAZAMA MATOKEO YA MOCK MKOA KIDATO CHA NNE July 07, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONDA ASHUHUDIA UTIAJI SAINI UJENZI WA BARABARA YA ESO - LONGDON NA UKUMBI WA MIKUTANO ARUSHA.

    April 03, 2025
  • RC MAKONDA ATAKA KUPEWA MAJINA YA WATENDAJI WANAOCHOCHEA MIGOGORO YA KIJAMII.

    March 28, 2025
  • KAMPENI YA MSAADA WA KISHERIA NI MAONO NA MAELEKEZO YA RAIS SAMIA- WAZIRI NDUMBARO.

    March 28, 2025
  • OFISI YA MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI YAFANYIA KAZI MALALAMIKO WANANCHI WA MIANZINI ARUSHA.

    March 28, 2025
  • Angalia Zote

Video

UZINDUZI WA BARABARA YA WASO-SALE
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • SALARY SLIP
  • Taarifa ya Mapato
  • Taarifa za Shule (SIS)
  • Takwimu za Sekta ya Elimu (BEMIS)
  • Video

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Portal ya Watumishi
  • Takwimu
  • TANAPA

Watembeleaji

world map hits counter

Wasiliana Nasi

Mawaliliano mengine

   

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani
    • Maswali ya Mara kwa Mara

Hatimiliki ©2018 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Arusha. Haki Zote Zimehifadhiwa