• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Arusha Regional

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Mkoa
      • Chimbuko/Asili ya eneo
      • Orodha ya wakuu wa Mikoa
    • Dira na dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji Mali
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Wilaya
    • Arusha
      • Historia
      • Viongozi
    • Arumeru
      • Historia
      • Viongozi
    • Monduli
      • Historia
      • Viongozi
    • Karatu
      • Historia
      • Viongozi
    • Longido
      • Historia
      • Viongozi
    • Ngorongoro
      • Historia
      • Viongozi
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Arusha
    • Halmashauri ya Arusha
    • Halmashauri ya Meru
    • Halmashauri ya Monduli
    • Halmashauri ya Karatu
    • Halmashauri ya Longido
    • Halmashauri ya Ngorongoro
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo
    • Viwanda
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Ardhi
    • Utalii
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali
    • Habari
    • Matukio

WANANCHI 604 WAJITIKOKEZA KUPATA  MATIBABU YA MOYO ARUSHA

Posted on: October 25th, 2024

WANANCHI 604 WAJITIKOKEZA KUPATA  MATIBABU YA MOYO ARUSHA

Na Prisca Libaga, Arusha

Jumla ya watu 604 wamepata huduma za uchunguzi na matibabu ya moyo zilizokuwa zinatolewa na wataalamu wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kwa kushirikiana na Arusha Lutheran Medical Centre (ALMC).

Akizungumza kuhusu kambi hiyo ya siku tano,  Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete, Dkt. Peter Kisenge alisema asilimia kubwa ya watu waliowaona walikuwa na tatizo la shinikizo la juu a damu.

Dkt. Kisenge ambaye pia ni daktari bingwa wa moyo na mishipa ya damu alisema kuna wagonjwa ambao waliwakuta na shida ya mfumo wa umeme wa moyo, misuli ya moyo kushindwa kufanya kazi  na kwa upande wa watoto waliwakuta na matatizo ya valvu na matundu.

“Katika kambi hii watu wote 604 tuliowaona tuliwafanyia vipimo vya kuangalia jinsi moyo unavyofanya kazi, mfumo wa umeme wa moyo na vipimo vya maabara.  Wagonjwa 83 wakiwemo watoto 21 tuliwakuta na matatizo ya moyo yaliyohitaji uchunguzi na matibabu zaidi hivyo basi tumewapa rufaa ya kuja kutibiwa JKCI”.

“Tumetoa elimu ya kufuata mtindo bora wa maisha ambao utawasaidia watu kutokupata magonjwa yasiyoambukiza yakiwemo ya moyo hii ikiwa ni pamoja na kufanya mazoezi, kula vyakula bora, kutokutumia bidhaa aina ya tumbaku na kutokunywa pombe kupitiliza pia tumetoa elimu ya matumizi sahihi ya dawa”, alisema Dkt. Kisenge.

Dkt. Kisenge alisema licha ya kutoa huduma za upimaji na matibabu kwa wananchi lakini pia wamewajengea uwezo wataalamu wa afya wa hospitali hiyo ambao kwa sasa wanaweza kuwatambua na kuwatibu wagonjwa wa moyo.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Magonjwa ya Moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Tatizo Waane alisema miundombinu iliyopo Arusha Lutheran Medical Centre (ALMC) iko vizuri na yote iko katika kuboresha afya ya watanzania na wananchi wa Arusha.

“Kambi hii ya matibabu hapa ALMC itakuwa endelevu, siku ya jumatatu (leo) madaktari wetu bingwa bobezi watakuwepo hapa wakitoa huduma kwa wananchi, ninawaomba wananchi mje kupima afya za mioyo yenu mapema  kwa kufanya hivi kwa wale watakaokutwa wagonjwa kutawapunguza madhara katika mioyo yao na kuepukana na gharama kubwa za matibabu"

Tangazo

  • TAZAMA MATOKEO YA MTIHANI WA MOCK MKOA DARASA LA SABA 1 July 06, 2023
  • MATOKEO YA MOCK MKOA DARASA LA SABA 2 July 07, 2023
  • TAZAMA MATOKEO YA MOCK MKOA KIDATO CHA NNE July 07, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONDA ASHUHUDIA UTIAJI SAINI UJENZI WA BARABARA YA ESO - LONGDON NA UKUMBI WA MIKUTANO ARUSHA.

    April 03, 2025
  • RC MAKONDA ATAKA KUPEWA MAJINA YA WATENDAJI WANAOCHOCHEA MIGOGORO YA KIJAMII.

    March 28, 2025
  • KAMPENI YA MSAADA WA KISHERIA NI MAONO NA MAELEKEZO YA RAIS SAMIA- WAZIRI NDUMBARO.

    March 28, 2025
  • OFISI YA MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI YAFANYIA KAZI MALALAMIKO WANANCHI WA MIANZINI ARUSHA.

    March 28, 2025
  • Angalia Zote

Video

UZINDUZI WA BARABARA YA WASO-SALE
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • SALARY SLIP
  • Taarifa ya Mapato
  • Taarifa za Shule (SIS)
  • Takwimu za Sekta ya Elimu (BEMIS)
  • Video

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Portal ya Watumishi
  • Takwimu
  • TANAPA

Watembeleaji

world map hits counter

Wasiliana Nasi

Mawaliliano mengine

   

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani
    • Maswali ya Mara kwa Mara

Hatimiliki ©2018 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Arusha. Haki Zote Zimehifadhiwa