• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Arusha Regional

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Mkoa
      • Chimbuko/Asili ya eneo
      • Orodha ya wakuu wa Mikoa
    • Dira na dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji Mali
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Wilaya
    • Arusha
      • Historia
      • Viongozi
    • Arumeru
      • Historia
      • Viongozi
    • Monduli
      • Historia
      • Viongozi
    • Karatu
      • Historia
      • Viongozi
    • Longido
      • Historia
      • Viongozi
    • Ngorongoro
      • Historia
      • Viongozi
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Arusha
    • Halmashauri ya Arusha
    • Halmashauri ya Meru
    • Halmashauri ya Monduli
    • Halmashauri ya Karatu
    • Halmashauri ya Longido
    • Halmashauri ya Ngorongoro
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo
    • Viwanda
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Ardhi
    • Utalii
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali
    • Habari
    • Matukio

WAZIRI GWAJIMA AHIMIZA JITIHADA ZAIDI, UKOMBOZI WA WANAWAKE DHIDI YA UKATILI.

Posted on: February 25th, 2025

Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi maalum, Dkt. Doroth Gwajima ameupongeza Mkoa wa Arusha kwa maandalizi mazuri kuelekea wiki ya wanawake duniani, akihimiza jitihada zaidi kwenye utekelezaji wa mikakati ya kuwainua wanawake katika nyanja mbalimbali pamoja na kuondoa unyanyasaji na ukatili wa aina mbalimbali kwa wanawake na wasichana.



Wakati akizungumza na wajumbe wa kamati mbalimbali za maandalizi ya maadhimisho ya Siku ya mwanamke duniani Machi 08, 2025, Waziri Dkt. Doroth Gwajima amesisitiza pia umuhimu wa Mkoa wa Arusha na mikoa mingine kote nchini, kuendelea kutoa elimu ya afya, Mikopo kwa wanawake sambamba na kuwafahamisha wananchi kuhusu fursa za uwezeshaji wanawake kiuchumi.



Akikemea udhalilishaji na ukatili wa kijinsia unaotokana na baadhi ya tamaduni katika Mikoa ya Arusha na Manyara inayopelekea ukeketaji kwa wasichana, Dkt. Gwajima amesisitiza umuhimu wa kubuniwa mikakati mbalimbali ya kutokomeza ukatili huo ili kubadilisha sura na takwimu za unyanyasaji katika Mikoa hiyo pamoja na kutokomeza fikra na tamaduni za kale zisizokuwa na faida kwa zama hizi.



Katika mazungumzo yao, Mhe. Makonda ameeleza kuwa Mkoa wa Arusha upo tayari kwaajili ya Siku ya mwanamke duniani ambapo maadhimisho yake Kitaifa yanatarajiwa kuwa Machi 08, 2025 Jijini Arusha na Kuongozwa na mgeni rasmi Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, akisema katika Juma la kuelekea Machi nane, shughuli mbalimbali zitafanyika ikiwemo elimu mbalimbali na utoaji wa elimu na msaada wa kisheria kwa wasichana na wanawake wa Mkoa wa Arusha pamoja na mashindano ya michezo ya aina mbalimbali kwaajili ya wanawake  kando ya burudani nyingine zitakazotolewa na wanawake ikiwemo mbio za magari na muziki kutoka kwa wanawake wanaounda bendi mbalimbali.



Kikao hicho pia kilichofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano kwenye Ofisi ya Mkuu wa mkoa wa Arusha, kilihudhuriwa na washauri wa Rais Mhe. Angellah Kairuki pamoja na Mhe. Sophia Mjema, Katibu tawala Mkoa wa Arusha Musa Missaile, wadau mbalimbali kutoka Taasisi za kifedha na wa masuala ya wanawake pamoja na Viongozi wengine wa Chama Cha Mapinduzi CCM na serikali.


Tangazo

  • TAZAMA MATOKEO YA MTIHANI WA MOCK MKOA DARASA LA SABA 1 July 06, 2023
  • MATOKEO YA MOCK MKOA DARASA LA SABA 2 July 07, 2023
  • TAZAMA MATOKEO YA MOCK MKOA KIDATO CHA NNE July 07, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONDA ASHUHUDIA UTIAJI SAINI UJENZI WA BARABARA YA ESO - LONGDON NA UKUMBI WA MIKUTANO ARUSHA.

    April 03, 2025
  • RC MAKONDA ATAKA KUPEWA MAJINA YA WATENDAJI WANAOCHOCHEA MIGOGORO YA KIJAMII.

    March 28, 2025
  • KAMPENI YA MSAADA WA KISHERIA NI MAONO NA MAELEKEZO YA RAIS SAMIA- WAZIRI NDUMBARO.

    March 28, 2025
  • OFISI YA MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI YAFANYIA KAZI MALALAMIKO WANANCHI WA MIANZINI ARUSHA.

    March 28, 2025
  • Angalia Zote

Video

UZINDUZI WA BARABARA YA WASO-SALE
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • SALARY SLIP
  • Taarifa ya Mapato
  • Taarifa za Shule (SIS)
  • Takwimu za Sekta ya Elimu (BEMIS)
  • Video

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Portal ya Watumishi
  • Takwimu
  • TANAPA

Watembeleaji

world map hits counter

Wasiliana Nasi

Mawaliliano mengine

   

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani
    • Maswali ya Mara kwa Mara

Hatimiliki ©2018 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Arusha. Haki Zote Zimehifadhiwa