• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Arusha Regional

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Mkoa
      • Chimbuko/Asili ya eneo
      • Orodha ya wakuu wa Mikoa
    • Dira na dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji Mali
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Wilaya
    • Arusha
      • Historia
      • Viongozi
    • Arumeru
      • Historia
      • Viongozi
    • Monduli
      • Historia
      • Viongozi
    • Karatu
      • Historia
      • Viongozi
    • Longido
      • Historia
      • Viongozi
    • Ngorongoro
      • Historia
      • Viongozi
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Arusha
    • Halmashauri ya Arusha
    • Halmashauri ya Meru
    • Halmashauri ya Monduli
    • Halmashauri ya Karatu
    • Halmashauri ya Longido
    • Halmashauri ya Ngorongoro
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo
    • Viwanda
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Ardhi
    • Utalii
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali
    • Habari
    • Matukio

WAZIRI MCHENGERWA AKABIDHI MAGARI 10 TSC, 9 YAPELEKWA OFISI ZA WILAYA

Posted on: August 13th, 2024

Ofisi ya Rais - Tamisemi 


Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais – Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Mhe. Mohamed Omary Mchengerwa amekabidhi magari 10 kwa Tume ya Utumishi wa Walimu (TSC) huku magari tisa (9) yakipelekwa katika ofisi za TSC ngazi ya Wilaya.


Akizungumza wakati wa hafla ya kukabidhi magari hayo iliyofanyika tarehe 11 Agosti, 2024 katika Ofisi za TAMISEMI Mtumba jijini Dodoma, Waziri Mchengerwa alisema kuwa Serikali inatambua kuwepo kwa  uhitaji mkubwa wa magari katika Ofisi za TSC 139 zilizopo katika kila wilaya nchini.


Alisema kuwa magari 10 yaliyotolewa ni mwanzo  wa kuanza kuboresha mazingira ya utendaji kwa Makatibu Wasaidizi ili waweze kutekeleza mjukumu yao kwa ufanisi.


“Ikumbukwe kuwa Serikali imekwisha toa magari kwa Makatibu Tawala Wasaidizi Seksheni ya Elimu wote nchini, Wakuu wa Divisheni za Elimu Msingi na Sekondari wote na sasa tumeanza kwa Makatibu Wasaidizi wa TSC wa Wilaya,” alisema.


Alisema lengo  la kutoa magari hayo ni kuimarisha usimamizi na ufuatiliaji wa shughuli za elimu zinazofanyika katika ngazi ya shule pamoja na kuwafikia walimu katika vituo vyao ili kuwasilikiliza na kutatua changamoto zinazowakabili.


Mhe. Mchengerwa alisema kuwa jukumu la usimamizi wa Elimu linahitaji uwajibikaji na usimamizi thabiti katika ngazi ya Taifa, Mikoa, Halmashauri, Kata na Shule.


Alisema kuwa pamoja na bidii, weledi, ubunifu, uaminifu na utiifu, mafanikio katika usimamizi wa elimu yanategemea pia uwezeshwaji wa vifaa na vitendea kazi ikiwemo vyombo vya usafiri.


Mhe. Mchengerwa aliongeza kuwa matarajio ya Serikali ni kuwa, magari waliyokabidhiwa yatakuwa nyenzo muhimu kwa viongozi wakiwemo Makatibu Wasaidizi  wa Wilaya katika usimamizi na ufuatiliaji wa Elimu nchini ikiwa ni pamoja na utatuzi wa kero zinazojitokeza.


Aidha , Waziri alielekeza kuwa magari hayo yatunzwe vizuri ili kuweza kuongeza ufanisi na ubora wa elimu katika utekelezaji wa majukumu ya kuwahudumia walimu ili wapite salama katika mzunguko wao wa ajira.


Tangazo

  • TAZAMA MATOKEO YA MTIHANI WA MOCK MKOA DARASA LA SABA 1 July 06, 2023
  • MATOKEO YA MOCK MKOA DARASA LA SABA 2 July 07, 2023
  • TAZAMA MATOKEO YA MOCK MKOA KIDATO CHA NNE July 07, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONDA ASHUHUDIA UTIAJI SAINI UJENZI WA BARABARA YA ESO - LONGDON NA UKUMBI WA MIKUTANO ARUSHA.

    April 03, 2025
  • RC MAKONDA ATAKA KUPEWA MAJINA YA WATENDAJI WANAOCHOCHEA MIGOGORO YA KIJAMII.

    March 28, 2025
  • KAMPENI YA MSAADA WA KISHERIA NI MAONO NA MAELEKEZO YA RAIS SAMIA- WAZIRI NDUMBARO.

    March 28, 2025
  • OFISI YA MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI YAFANYIA KAZI MALALAMIKO WANANCHI WA MIANZINI ARUSHA.

    March 28, 2025
  • Angalia Zote

Video

UZINDUZI WA BARABARA YA WASO-SALE
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • SALARY SLIP
  • Taarifa ya Mapato
  • Taarifa za Shule (SIS)
  • Takwimu za Sekta ya Elimu (BEMIS)
  • Video

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Portal ya Watumishi
  • Takwimu
  • TANAPA

Watembeleaji

world map hits counter

Wasiliana Nasi

Mawaliliano mengine

   

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani
    • Maswali ya Mara kwa Mara

Hatimiliki ©2018 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Arusha. Haki Zote Zimehifadhiwa