• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Arusha Regional

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Arusha

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia ya Mkoa
      • Chimbuko/Asili ya eneo
      • Orodha ya wakuu wa Mikoa
    • Dira na dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji Mali
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Maji
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Manunuzi na Ugavi
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Wilaya
    • Arusha
      • Historia
      • Viongozi
    • Arumeru
      • Historia
      • Viongozi
    • Monduli
      • Historia
      • Viongozi
    • Karatu
      • Historia
      • Viongozi
    • Longido
      • Historia
      • Viongozi
    • Ngorongoro
      • Historia
      • Viongozi
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Arusha
    • Halmashauri ya Arusha
    • Halmashauri ya Meru
    • Halmashauri ya Monduli
    • Halmashauri ya Karatu
    • Halmashauri ya Longido
    • Halmashauri ya Ngorongoro
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Ufugaji
    • Kilimo
    • Viwanda
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Ardhi
    • Utalii
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali
    • Habari
    • Matukio

RC MONGELLA ALIA NA WAHUDUMU WA AFYA; AWATAKA KUTOA HUDUMA BORA KWA WAGONJWA...

Posted on: November 7th, 2023

Na Elinipa Lupembe

Mkuu wa mkoa wa Arusha Mhe. John V.K. Mongella amewataka watalamu wanaotoa huduma za afya kutoa huduma bora na stahiki kwa wagonjwa ili kuhakikisha wanapona na zaidi kufikia lengo la serikali la kupunguza idadi ya vifo visivyo vya lazima hususani kwa kina wajawazito na watoto wa chini ya miaka mitano.

Ametoa rai hiyo wakati akikagua dawa na vifaa tiba, vilivyoletwa na serikali mara baada ya kukamilika asilimia kubwa  ya majengo kwenye Hospitali mpya ya wilaya ya Longido.

Mhe. Mongella amewataka Watoa huduma za Afya kufanya kazi kwa weledi kwa ya kuwahudumia wagonjwa kwa kuwa serikali imewekeza fedha nyingi katika ujenzi wa miundombinu pamoja wa ununuzi wa vifaa tiba.

Wahudumu wa afya mnapaswa kuzingatia nia ya serikali ya kuwekeza kwenye miundombinu hii ya afya ya kuhakikisha utoaji na upatikanaji wa huduma bora kwa wananchi, hivyo ni jukumu lenu kutimiza wajibu wenu ili kufikia lengo la serikali kwa kuwa mmepewa dhamana hiyo muhimu ya maisha ya watu.

"Mhe Rais anahangaika kutafuta fedha, fedha ambazo zimetolewa kujenga hospitali hii pamoja na dawa na vifaa tiba, hakikisheni kila mtumishi anatimiza wajibu wake ili wananchi wavutike kutumia huduma kwenye hospitali zetu za serikali, haiwezekani mwananchi ateseke wakati serikali yake imeshaandaa miundombinu bora ya kumpa huduma bora" Amesisitiza Mhe. Mongella

Ameongeza kuwa endapo mtatoa huduma bora mtawapunguzia wananchi gharama za kwenda hospitali ya Mount Meru na pia itapunguza msongamano wa wagonjwa waliokuwa wanafuata huduma Mount Meru na kuongeza kuwa serikali inataka kila mwananchi apate huduma zote ndani ya eneo analoishi jambo ambalo licha ya kupunguza gharama litaongeza utunzaji wa muda kwa wananchi wa kutafuta huduma za afya mbali.

Mradi huo umetekelezwa na Serikali kwa gharama ya shilingi Bilioni 3.4, ambapo shilingi Bilioni 3 ni fedha kutoka Serikali Kuu hukunshilingi milioni 340 ni kupitia fedha za mapambano dhidi ya Ugonjwa wa UVIKO 19.

Aidha hospitali hiyo inategemea kuhudumia zaidi ya wagonjwa 175,915 wa wilaya ya Longido na wengine kutoka Nchi jirani ya Kenya, kukiwa na lengo la kutoa huduma zote za afya pamoja na kupungumza gharama kwa wagonjwa kusafiri mpaka Hospitali ya Rufaa ya Mount Meru jijini Arusha, sambamba na kupunguza msongamano wa wagonjwa katika hospitali hiyo ya Rufaa.

Ikumbukwe kuwa ujenzi wa hospitali za wilaya ni utekelezaji wa Ilani ya Chama cha Mapinduzi CCM wa kuhakikisha kila Wilaya inakuwa na Hopitali kwa lengonla kusongeza huduma muhimu karibu na wananchi ikiwa na mapngo maalum wa kupambana na kuzuia vifo vya mama na mtoto wakati wa kujifungua.



#arushafursalukuki
#kaziinaendelea


Tangazo

  • TAZAMA MATOKEO YA MTIHANI WA MOCK MKOA DARASA LA SABA 1 July 06, 2023
  • MATOKEO YA MOCK MKOA DARASA LA SABA 2 July 07, 2023
  • TAZAMA MATOKEO YA MOCK MKOA KIDATO CHA NNE July 07, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONDA ASHUHUDIA UTIAJI SAINI UJENZI WA BARABARA YA ESO - LONGDON NA UKUMBI WA MIKUTANO ARUSHA.

    April 03, 2025
  • RC MAKONDA ATAKA KUPEWA MAJINA YA WATENDAJI WANAOCHOCHEA MIGOGORO YA KIJAMII.

    March 28, 2025
  • KAMPENI YA MSAADA WA KISHERIA NI MAONO NA MAELEKEZO YA RAIS SAMIA- WAZIRI NDUMBARO.

    March 28, 2025
  • OFISI YA MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI YAFANYIA KAZI MALALAMIKO WANANCHI WA MIANZINI ARUSHA.

    March 28, 2025
  • Angalia Zote

Video

UZINDUZI WA BARABARA YA WASO-SALE
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA Serikalini
  • SALARY SLIP
  • Taarifa ya Mapato
  • Taarifa za Shule (SIS)
  • Takwimu za Sekta ya Elimu (BEMIS)
  • Video

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Portal ya Watumishi
  • Takwimu
  • TANAPA

Watembeleaji

world map hits counter

Wasiliana Nasi

Mawaliliano mengine

   

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani
    • Maswali ya Mara kwa Mara

Hatimiliki ©2018 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Arusha. Haki Zote Zimehifadhiwa